Saturday, June 3, 2017

Tetesi Mpya Za Usajili Manchester United

Tetesi za usajili katika klabu ya Manchester United.


Man United Kukamilisha Uhamisho Wa Lacazette
klabu ya Manchester United ipo mbioni kuhakikisha inamsajili straika wa Lyon Alexandre Lacazette, kwa mujibu wa L'Equipe

Man United Yatupilia Mbali Ofa ya Paundi Milioni 60 ya Real Madrid Kumtaka De Gea
Manchester United imekataa ofa ya paundi milioni 60 iliyotolewa na klabu ya Real Madrid ikihitaji kupata huduma ya mlinda mlango David De Gea, kwa mujibu wa Sky Sports News

Mourinho Amfukuzia Morata Kimyakimya
Jose Mourinho amekuwa katika mawasiliano binafsi na straika wa Real Madrid Alvaro Morata, kwa mujibu wa OkDiario

Bale katika Rada ya Man U
Man U inaendelea kumfuatilia kwa ukaribu Winga wa Real Madrid Gareth Bale, kwa mujibu wa Mundo Deportivo Reports

Lindelof Kuigharimu Man Utd paundi milioni 52
Man U wameambiwa wanatakiwa kutoa kitita cha paundi milioni 52 kumnasa beki wa Benifica Victor Lindelof, kwa mujibu wa A Bola

Man Utd Yaongoza Mbio Za Kumuwania Rose
Man Utd inaongoza katika mbio za kuipata saini ya Beki wa Tottenham Danny Rose, kwa mujibu wa Daily Mirror.

Herrera Kutupilia Mbali Dili la Barcelona
Inaonekana wazi kuwa Ander Herrea atalikataa dili la Barcelona na kuendelea kusalia katika klabu ya Man U.

Lukaku katika Rada za Mourinho
Straika wa Everton Romelu Lukaku anawaniwa na klabu za Chelsea na Man United kwa mujibu wa Express.

Related Posts:

  • HUYU NDO KOCHA MPYA BRAZILTite ametajwa kuwa kocha mpya wa Brazil baada ya Dunga kutupiwa virago kufuatia matokeo mabovu waliyoyapata Brazil Copa America 2016. Tite Tite 55, anachukua nfasi ya Dunga aliyetimuliwa mara baada ya Brazil kutolewa hatu… Read More
  • MATARAJIO YA SIMBA KIKOSI KIPYA MSIMU UJAOZacharia Hans Poppe, mwenyekiti wa kamati ya usajili Simba, amesem a kikosi chao msimu ujao kitakuwa na mabadiliko makubwa kuanzia benchi la ufundi hadi wachezaji. Simba kwa sasa ipo katika harakati za kuhakikisha wanawana… Read More
  • KIFAA KIPYA YANGA KUTUA LEO JANGWANIWalter Musona Mshambuliaji kutoka FC Platinum ya Zimbabwe anatarajiw kuwasili Daresalaam leo alasiri kwa ajili ya mazungumzo na klabu ya Yanga. Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika kutoka katika klabu ya Yanga, tayari mambo yo… Read More
  • RUVU SHOOTING KUKIPA NGUVU KIKOSI CHAORuvu Shooting ipo katika mipango ya kusajili wachezaji saba ili kujiimarisha kabla hawajaanza kipute cha ligi kuu Vodacom msimu wa 2016/17. kwa sasa Ruvu Shooting inaendelea na kambi kwenye uwanja wa Mabatini Mlandizi, Pwa… Read More
  • KOCHA MWENYE REKODI ZA KIMATAIFA KUTUA SIMBAHarakati za usajili katika klabu ya Simba bado zinaendelea na habari za hivi karibuni zinasema makocha wanne kutoka katika nchi nne tofauti wamejitokeza kutaka kuinoa klabu hiyo. Geofrey Nyange "Kaburu" (Makamu mwenyekiti … Read More

0 comments:

Post a Comment