Mlinda mlango wa Liverpool
Simon Mignolet ameonekana kuwaangusha mamilioni ya mashabiki wa
Liverpool msimu huu na kocha Klopp anafikiria kumleta kipa mwingine anayechezea
Barcelona kwa sasa Marc-Andre ter Stegen.
Mlinda mlango huyo wa Barcelona anayesifiwa sana kwa kiwango
chake alichoonyesha klabuni hapo tangu alipojiunga mwaka 2014, amekuwa katika
mipango ya Jurgen Klopp ili kuimarisha kikosi chake katika nafasi hiyo ya
mlinda mlango.
Alipoulizwa hivi karibuni kuwa yeye anafikiri ni kipa gani
Louis Enrique atakuwa na mipango nae ya baadae, Ter Stegen alisema “Sijui
kocha anachokifikiria” Comment ambayo imeongeza hisia kuwa huenda mlinda mlango
huyo akawashiwa taa nyekundu klabuni hapo, kwani licha ya kufanya vizuri na
kudhihirisha uwezo wake mkubwa klabuni hapo, Ter Stegen amecheza katika mechi 4
tu katika mechi zote za ligi msimu huu, huku Claudio Bravo akionekana kuwa ndo chaguo namba
moja la Enrique.
Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com
0 comments:
Post a Comment