Yanga Yainyoosha Azam Fc Chamanzi

Azam FC 1 - 2 Young Africans.

Kiungo Wa Everton James McCathy Avunjika Mguu

Kiungo James McCarthy wa Everton sasa atakaa nje na kuukosa msimu wote huh baada ya kuvunjika mifupa miwili ya mguu wake.

DRAW CAF CL And CC 2018

Draw Caf Cl and CC 2018

Yanga Yazinduka Yaambulia Ushindi Mwembamba

Klabu ya Yanga leo imefanikiwa kuibuka na ushindi mwembamba wa goli moja kwa sifuri

Madrid Yaivurumisha Deportivo 7-1

Klabu ya Real Madrid leo imefanikiwa kuchomoza na ushindi mnono kwa jumla ya magoli 7-1 dhidi ya Klabu Deportivo la Coruna

Showing posts with label Bundesliga. Show all posts
Showing posts with label Bundesliga. Show all posts

Saturday, October 22, 2016

RATIBA YA MICHEZO MBALIMBALI DUNIANI LEO OCTOBER 22



RATIBA LIGI KUU MBALIMBALI DUNIANI
TANZANIA Vpl october 22
16:00       Kagera Sugar  vs Young Africans
16:00       African Lyon vs Mbeya City
16:00       Ndanda Fc vs Mwadui
16:00       Mtibwa Sugar vs Stand United
16:00      Majimaji vs Ruvu Shooting
19:00      Azam FC vs JKT Ruvu
ENGLAND EPL October 22
14:30      AFC Bournemouth vs Tottenham Hotspur
17:00      Arsenal vs Middlesbrough
17:00      Burnley vs Everton
17:00      Hull City vs Stoke City
17:00      Leicester City vs Crystal Palace
17:00      Swansea City vs Watford
17:00     West Ham United vs Sunderland
19:30      Liverpool vs West Bromwich Albion
ITALY - Serie A October 22
19:00       Sampdoria vs Genoa
21:45        AC Milan vs Juventus
SPAIN - LaLiga Santander October 22
14:00          Espanyol vs Eibar
17:15         Valencia vs Barcelona
19:30         Real Sociedad vs Alaves
21:45         Granada vs Sporting Gijon
GERMANY - Bundesliga October 22
16:30            Bayer Leverkusen vs Hoffenheim
16:30            Darmstadt vs Wolfsburg
16:30            Freiburg vsAugsburg
16:30            Hertha Berlin vs FC Cologne
16:30            Ingolstadt vs Borussia Dortmund
19:30            Bayern Munich vs Borussia Moenchengladbach         
FRANCE - Ligue 1 October 22
18:00         Lyon vs Guingamp
21:00        Angers vs Toulouse
21:00        Bordeaux vs Nancy
21:00        Dijon vs Lorient
21:00        Lille vs SC Bastia
21:00       Nantes vs Rennes
KENYA - Premier League October 22
14:00       Mathare United vs Bandari

15:00      Kakamega Homeboyz vs SoNy Sugar

Sunday, October 16, 2016

MATOKEO YA MICHEZO MBALIMBALI ILIYOFANYIKA JANA NI KAMA IFUATAVYO

Sunday, October 2, 2016

RATIBA EPL LEO JUMAPILI 2 OCTOBER 2016


Saturday, June 4, 2016

PIERRE-EMERICK AUBAMEYANG AMBWAGA LEWANDOWSKI TUZO ZA MCHEZAJI BORA BUNDESLIGA 2015/16

Mchezaji kandanda bora barani Afrika wa mwaka huu Pierre-Emerick Aubameyang ametawazwa kuwa mshindi wa tuzo la mwaka huu la mchezaji bora katika ligi kuu ya Ujerumani Bundesliga.


Sunday, May 15, 2016

STUTTGART 3 ZASHUKA DARAJA MSIMU HUU


Msimu wa ligi wa 2015/16 umekuwa msimu mbaya kwa wakazi wa jiji la Stuttgart  katika tasnia ya mpira wa miguu. Timu tatu za Stuttgart zimeshuka daraja katika ligi zote 3 zikizoshiriki, Stuttgart iliyokuwa inashiriki ligi kuu kwa maana Bundesliga, Stuttgart II ya ligi daraja la kwanza na Stuttgarter Kickers waliokuwa katika ligi daraja la pili.

Timu  hizo zote zimejikuta zikishuka daraja katika ligi walizokuwa wanashiriki, Stuttgart iliyokuwa katika ligi kuu wameshuka daraja rasmi baada ya mchezo wao wa mwisho wa ligi kuu waliokubali kipigo cha magoli 3 – 1, mabingwa hao wa Bundesliga msimu wa 2007 wameshuka daraja baada ya kudumu katika ligi kuu kwa takribani miaka 39 bila kushuka daraja.
Stuttgart II tayari wao walishashuka daraja hata kabla ya mchezo wao wa mwisho na Stuttgarter Kickers wao wameshuka daraja baada ya kukubali kichapo katika uwanja wao wa nyumbani cha goli 1 – 0 kutoka kwa Cheminitzer FC .

LEWANDOWSKI AIFIKIA REKODI ILIYOWEKWA MIAKA 39 ILIYOPITA


MCHEZAJI wa zamani wa klabu ya Borrusia Dortmund anayekipiga katika klabu ya Bayern Munich kwa sasa Robert Lewandowski amefikia rekodi iliyowekwa miaka 39 iliyopita katika ligi kuu nchini Ujerumani maarufu kama Bundesliga.

Robert Lewandowski amethibitisha ubora wake katika ligi ya Ujerumani Bungesliga akifanikiwa kufunga magoli 30 baada ya mchezo ambao Bayern walicheza na Hannover siku ya jumamosi na kuibuka na ushindi wa magoli 3 - 1.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Poland amempiku staa wa Dortmund Pierre-emerick Aubameyang katika mbio za kuwania tuzo ya mfungaji bora wa ligi kwa kufikisha magoli 30 akifikia pia rekodi iliyowekwa mwaka 1977 ya mchezaji asiye Mjerumani kufikisha idadi ya magoli 30 katika msimu mmoja wa ligi kuu nchini Ujerumani,  huku Aubameyang akiwa na magoli 25.
Koln’s Dieter Muller alilkuwa mchezaji wa mwisho kufikisha idadi ya magoli 30 akifunga magoli 34 katika msimu wa 1976/77 huku timu yake ikimaliza katika nafasi ya 5 katika msimamo wa ligi

Gerd Muller yeye ndo anashikilia rekodi ya ufungaji katika ligi ya Ujerumani akifanikiwa kufunga jumla ya magoli 40 katika msimu mmoja.

Saturday, May 7, 2016

BAYERN MUCHEN MABINGWA BUNDESLIGA 2015/16



Bayern Muchen wametwaa ubingwa kwa mara ya nne mfululizo baada ya kuichapa Ingolstadt kwa jumla ya magoli 2 - 1. Bayern wametwaa ubingwa huo kwa mara ya 27 katika ligi kuu ya Nchini Ujerumani. Magoli yaliyofungwa dakika ya 15 na 32 na mshambuliaji wa kimataifa wa Poland, Lewandowski yametosha kuipa ushindi Bayern huku Lewandowski mwenyewe akiwa katika chati ya Wafungaji bora wa ligi hiyo akiwa amefunga magoli 29 katika ligi huku akifuatiwa na Aubameyang wa Borussia Dortmund aliyepachika magoli 25.

Matokeo Mengine Mechi za Leo May 7,Ligi kuu Ujeruman- Bundesliga.

M'gladbach 2 - 1 Bayer Leverkusen

Frankfurt 1 - 0 Dortmund

Hamburger SV 0 - 1 Wolfsburg

Hannover 96 1 - 0 Hoffenheim

Hertha 1 - 2 Darmstadt

Köln 0 - 0 Werder Bremen

Schalke 04 1 - 1 Augsburg


Stuttgart 1 - 3 Mainz

Sunday, May 1, 2016

BORUSSIA M’GLADBACH WAHARIBU SHEREHE ZA UBINGWA WA BAYERN MUCHEN


Vijana wa Pep Guardiola walizuiwa kusherehekea ushindi wao wa 4 Mfululizo baada ya kulazimishwa sare na Borussia Monchengladbach, mchezo uliopigwa katika uwanja wa Allianz Arena jana.

Andre Hahn alisitisha sherehe za ubingwa wa Bundesliga kwa mara ya 4 Mfululizo baada ya kuisawazishia timu yake goli dakika ya 72, baada ya Thomas Muller kuifungia Bayern goli dakika ya 6’ ya mchezo. Bayern endapo wangeshinda mechi hiyo wangetawazwa rasmi mabingwa wapya wa Bundesliga msimu 2015/2016,  hivyo watatakiwa kusubiri wiki moja baadae katika mchezo wao na Ingolstadt utakaopigwa siku ya May 7 ambapo wakishinda watakuwa mabingwa tena kwa mara ya 4.

Kwa sasa wako mbele kwa tofauti ya pointi 5 na Borussia Dortmund ambao wameibuka na ushindi wa magoli 5 – 1 dhidi ya Wolfsburg hiyo hiyo jana.




Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

Tuesday, April 26, 2016

Liverpool Na Dortmund Vitani Kuwania Saini Ya Gotze


Uongozi wa klabu ya Liverpool unaamini uwepo wa Jurgen Klopp klabuni hapo huenda ukaamua hatima ya Mario Gotze Msimu ujao. Gotze anaeonekana kuto kupata nafasi kwa sasa katika klabu ya Bayern anawindwa huenda akaondoka klabuni hapo mwishoni mwa msimu huu.

Liverpool na Borussia Dortmund watapambana katika kuinasa saini ya mchezaji huyo.p. Liverpool wanaonekana kumhitaji mchezaji huyo ambae amewahi kutwaa kombe la dunia akiwa na Timu yake ya Taifa ya Ujerumani mwaka juzi lakini Dortmund nao wamethibitisha kumuhitaji mchezaji wao huyo wa zamani.

Gotzea alijiunga na Bayern mwaka 2013 akitokea Dortmund kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 32. Kuondoka kwake kuliwaudhi sana mashabiki wa Dortmund kwani alitoa kauli ya kutaka kujiunga na Bayern siku chake kabla ya mechi yao ya nusu fainali ya UEFA dhidi ya Real Madrid. Wiki mbili baadae Dortmund na Bayern zilikutana katika fainali ya UEFA Champions League katika uwanja wa Wembly, fainali ambayo Gotze aliikosa kutokana na kuwa majeruhi.

Mtendaji Mkuu wa Dortmund Hans-Joachim Watzke amethibitisha kuwa klabu inamuhitaji Gotze lakini atatakiwa kutoa maelezo ya kwanini aliondoka klabuni hapo. 

Akiongea na waandishi wa habari Watzke alisema “Kama yupo sokoni (Gotze), ni wazi kuwa tutakaa kumjadili, Mlango uko wazi kwa mchezaji yoyote anehitaji kujiunga na Dortmund”.

Mabango yametandazwa na mashabiki katika uwanja wa Dortmund yanayoashiria kumdharau Gotze, lakini Watzke anaamini mashabiki wanaweza kutulizwa na kusahau yaliyopita na kumpa nafasi nyingine Gotze.

Watzke Aliongeza kwa kusema “kama akirudi Dortmund, tutazungumza na mashabiki na Gotze atatakiwa kuwaambia mashabiki ni kwanini aliondoka klabuni hapo na kujiunga na Bayern”

Upande wa pili Klopp anamuona Gotze kuwa ndo kipaumbele chake cha kwanza katika msimu ujao wa usajili.


Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

Wednesday, April 6, 2016

"MARIO GOTZE ATAKUWA MJINGA KWENDA LIVERPOOL"

Supastaa wa Bayern Munich Robert Lewandowski amemshauri Mario Gotze kukataa ofa yoyote Liverpool watakayompa kwa usajili wa majira ya joto

Mcheka na nyavu huyo wa Poland anaamini Gotze anaweza kuthibiti kama moja ya wachezaji bora dunia kama akiendelea kubaki na klabu hiyo ya Bundesliga.

Jurgen Klopp anataka kuungana na mchezaji hyo Liverpool lakini Lewandowski ametoa mtazamo wake juu ya hali hiyo.

Alikiambia Liverpool Echo: “Mario ameonyesha kipindi cha mapumziko ya kimataifa kuwa anaweza kufanya mambo makubwa na ni mchezaji mahiri.

 “Hapaswi kufuata kile wasemacho watu kuhusu yeye kwenye magazeti. Hahitaji msukumo wa ziada.

“Hata hivyo Mario anajua kufanya maamuzi ya busara. Tetesi nyingu juu yake ni kero hata hivyo.

“Ni mchezaji wa Bayern na bado ana mechi nyingi mbele yake hadi mwisho wa msimu kuthibitisha ana ubora wa kuichezea Bayern.

“Ana muda wa kutosha kukanusha wanaodai kiwango chake ni dhaifu. Abaki Bayern kwa muda zaidi kwa sababu ni mchezaji bora.”