Thursday, March 2, 2017

Liverpool Vs Arsenal, historia, uchambuzi na utabiri


MUDA: 20:30

UWANJA: ANFIELD,LIVERPOOL

Liverpool wanawaalika Arsenal katika dimba la Anfield wikiendi hii wakiwa na rekodi nzuri ya mechi mchezo wa kwanza uliofanyika Emirates ambapo walishinda 4 – 3 dhidi ya Arsenal kwa magoli ya Coutinho (45'+1, 56’), Lallana (49'), Mané (63') wakati yale ya Arsenal yalifungwa na Walcott (31'), Oxlade-Chamberlain (64'), Chambers (75').



Liverpool pia wanaingia uwanjani jumamosi wakiwa na kazi moja tu ya kuhakikisha wanashinda Kutokana na shinikizo la Manchester United ambayo inaonekana kuimarika ikiwa nyuma kwa alama 1 tu.

Mchezo wa mwisho wa Liverpool ilikubali kipigo kikali toka kwa bingwa mtetezi wa ligi hiyo Leicester City cha goli 3 – 1.

Mchezo wa jumamosi unakuwa na hamasa ya aina yake kwani timu hizo mbili zinapishana pointi moja tu Liverpool wanapointi 49 baada ya michezo 26 katika nafasi ya 5 huku Arsenal wakiwa na pointi 50 katika michezo 25.

Liverpool na Arsenal tangu mwaka 2010 wamekutana mara 13, Arsenal wameshinda mara nyingi zaidi mara 4 wakati Liverpool wameshinda mara 3 na kutoka suluhu mara 6.

Jumla ya magoli 45 yamefungwa katika michezo hiyo na vipigo vikubwa ni 08 Feb 2014 Liverpool 5 Arsenal 1 katika dimba la Anfield.

04 Apr 2015 Arsenal 4 Liverpool 1katika dimba la Emirates.

Zifuatazo ni rekodi za Liverpool na Arsenal katika ligi kuu tangu 2010

15 Aug 2010   Liverpool v Arsenal    1-1       Premier League 2010/2011
17 Apr 2011    Arsenal v Liverpool    1-1       Premier League
20 Aug 2011   Arsenal v Liverpool    0-2       Premier League 2011/2012
03 Mar 2012    Liverpool v Arsenal    1-2       Premier League
02 Sep 2012    Liverpool v Arsenal    0-2       Premier League 2012/2013
30 Jan 2013     Arsenal v Liverpool    2-2       Premier League
02 Nov 2013   Arsenal v Liverpool    2-0       Premier League 2013/2014
08 Feb 2014    Liverpool v Arsenal    5-1       Premier League
21 Dec 2014    Liverpool v Arsenal    2-2       Premier League 2014/2015
04 Apr 2015    Arsenal v Liverpool    4-1       Premier League
24 Aug 2015   Arsenal v Liverpool    0-0       Premier League 2015/2016
13 Jan 2016     Liverpool v Arsenal    3-3       Premier League
14 Aug 2016   Arsenal v Liverpool    3-4       Premier League   2016/2017

4 March 2017  Liverpool vs Arsenal      ?       Premier League   

Related Posts:

  • MAISHA YA FABREGAS CHELSEA YAFIKA UKINGONI Cesc Fabregas ameambiwa na kocha wa klabu ya Chelsea Antonio Conte kuwa anaweza kuondoka klabuni hapo. Conte ametoa kauli hiyo huku kukiwa kumebaki siku 2 tu kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili barani ulaya. Kiungo h… Read More
  • DAVID MOYES AWANASA WAWILI KUTOKA MANCHESTER UNITED Boss Mpya wa klabu ya Sunderland, David Moyes amekamilisha usajili wa wachezaji wawili kutoka katika klabu ya Manchester United. Klabu ya Manchester United imethibitisha kuuzwa kwa wachezaji wao wawili ambao ni Paddy McNa… Read More
  • VIDEO: INTERVIEW YA KWANZA YA DAVID MOYES SUNDERLAND David Moyes ameteuliwa kuwa kocha mkuu wa klabu ya Sunderland akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Sam Allardyce aliyekabidhiwa timu ya taifa ya Uingereza. Hii hapa chini Interview Yake ya kwanza mara tu baada ya kutang… Read More
  • CLAUDIO RANIERI AIONYA MAN UNITEDClaudio RanieriKocha Wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu nchini Uingereza Leicester City, Claudio Ranieri ameionya Man United kuwa wasitegemee mchezo rahisi leo. Ranieri amedai anaamini kuna kitu kizuri kinakuja katika klabu yak… Read More
  • RASMI: MANCHESTER CITY YAMNASA MORENO Klabu ya Manchester City iliyo chini ya kocha Mpya Pep Guardiola imekamilisha uhamisho wa kinda Mkolombia Marlos Moreno. Moreno 19, ametua katika dimba la Etihad akitokea Atletico Nocional na amesaini mkataba wa miaka mit… Read More

0 comments:

Post a Comment