Saturday, June 3, 2017

Tetesi Mpya Za Usajili Arsenal

Ungana na Soka24, kwa habari za papo kwa papo za usajili katika klabu kubwa na pendwa zaidi duniani, hapa nimekuwekea yanayojiri katika klabu ya Arsenal hivi sasa.


Arsenal katika mbio za Kumuwania Mbappe
klabu ya Arsenal imeingia katika vita ya kuiwania saini ya nyota wa Monaco Kylian Mbappe, kwa mujibu wa L'Equipe

Juve Yamtolea Macho Szczesny
Wojchiech Szczesny anaweza kuendelea kubaki katika ligi ya Italia Serie A baada ya Juve kutenga kitita cha paundi milioni 14 kwa mlinda mlango huyo wa Arsenal aliyepo kwa mkopo, kwa mujibu wa Daily Mail.

Wenger Aonywa kuhusu Usajili
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger huenda akaonywa aache kusitasita katika kufanya usajili kuelekea kikao cha bodi cha klabu hiyo, kwa mujibu wa Daily Mail.

Wenger Aahidiwa Paundi Milion 100
Arsene Wenger atakabidhiwa kitita cha paundi milioni 100 azitumie katika kuimarisha kikosi chake kwenye kipindi hiki cha usajili endapo atasaini mkataba mpya, kwa mujibu wa Daily Star.

Arsenal Yaongoza Mbio za kumuwania Belotti.
klabu ya Arsenal imeonyesha nia ya kuhitaji huduma ya Andrea Belotti akitokea Torino, kwa mujibu wa The Sun.

Arsenal Yampa Ofa Nono Sanchez
klabu ya Arsenal imempa ofa ya mkataba mpya nyota wake Alexis Sanchez wenye thamani ya paundi 270,000 kwa wiki endapo atakuwa tayari kubaki klabuni hapo, huku Bayern Munich ikiwa imeshaonesha nia ya kumsajili mchezaji huyo, kwa mujibu wa Daily Mail.

0 comments:

Post a Comment