Saturday, June 3, 2017

Tetesi Mpya Za Usajili Arsenal

Ungana na Soka24, kwa habari za papo kwa papo za usajili katika klabu kubwa na pendwa zaidi duniani, hapa nimekuwekea yanayojiri katika klabu ya Arsenal hivi sasa.


Arsenal katika mbio za Kumuwania Mbappe
klabu ya Arsenal imeingia katika vita ya kuiwania saini ya nyota wa Monaco Kylian Mbappe, kwa mujibu wa L'Equipe

Juve Yamtolea Macho Szczesny
Wojchiech Szczesny anaweza kuendelea kubaki katika ligi ya Italia Serie A baada ya Juve kutenga kitita cha paundi milioni 14 kwa mlinda mlango huyo wa Arsenal aliyepo kwa mkopo, kwa mujibu wa Daily Mail.

Wenger Aonywa kuhusu Usajili
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger huenda akaonywa aache kusitasita katika kufanya usajili kuelekea kikao cha bodi cha klabu hiyo, kwa mujibu wa Daily Mail.

Wenger Aahidiwa Paundi Milion 100
Arsene Wenger atakabidhiwa kitita cha paundi milioni 100 azitumie katika kuimarisha kikosi chake kwenye kipindi hiki cha usajili endapo atasaini mkataba mpya, kwa mujibu wa Daily Star.

Arsenal Yaongoza Mbio za kumuwania Belotti.
klabu ya Arsenal imeonyesha nia ya kuhitaji huduma ya Andrea Belotti akitokea Torino, kwa mujibu wa The Sun.

Arsenal Yampa Ofa Nono Sanchez
klabu ya Arsenal imempa ofa ya mkataba mpya nyota wake Alexis Sanchez wenye thamani ya paundi 270,000 kwa wiki endapo atakuwa tayari kubaki klabuni hapo, huku Bayern Munich ikiwa imeshaonesha nia ya kumsajili mchezaji huyo, kwa mujibu wa Daily Mail.

Related Posts:

  • PSG Wakubali Yaishe Kwa Aubameyang Vigogo wa soka nchini Ufaransa, PSG wamekubali kutoa paundi milioni 61 kuinasa saini ya mshambuliaji wa Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang. Licha ya gharama hizo za uhamisho PSG pia wamekubali kumlipa nyota huyo kutoka b… Read More
  • Simba Wapata Mbadala Wa Juuko Murshid Munezero Fiston ni Mnyarwanda ambaye yupo katika mipango ya Simba baada ya kocha Joseph Omog kupendekeza atafutiwe mchezaji mwingine. Munezero, anayekipiga katika klabu ya Rayon Sport anatarajiwa kutua Dar Es Salaam Juma… Read More
  • Tetesi Mpya Za Usajili Manchester United Tetesi za usajili katika klabu ya Manchester United. Man United Kukamilisha Uhamisho Wa Lacazette klabu ya Manchester United ipo mbioni kuhakikisha inamsajili straika wa Lyon Alexandre Lacazette, kwa mujibu wa L'Equipe … Read More
  • Ozil, Sanchez Washusha Presha Ya Mashabiki Arsenal Washambuliaji machachari wa klabu ya Arsenal Mesut Ozil na Alexis Sanchez wameshusha presha ya mashabiki wengi wa Arsenal baada ya uvumi kuenea kuwa nyota hao wataihama klabu hiyo. Taarifa za hivi punde zinadai kuwa wach… Read More
  • Tetesi Mpya Za Usajili Arsenal Ungana na Soka24, kwa habari za papo kwa papo za usajili katika klabu kubwa na pendwa zaidi duniani, hapa nimekuwekea yanayojiri katika klabu ya Arsenal hivi sasa. Arsenal katika mbio za Kumuwania Mbappe klabu ya Arsenal… Read More

0 comments:

Post a Comment