Saturday, May 21, 2016

DENIS KITAMBI KATIKA MTIHANI MZITO AZAM FC

Kocha Msaidizi wa Azam FC  Denis Kitambi Ataiongoza klabu hiyo katika mchezo wa mwisho wa Ligi katika kuwania nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu Tanzania Bara.


Ligi Kuu Tanzania Bara inaelekea ukingoni na mechi za mwisho zitachezwa Jumapili hii Mei 22. Azam FC itashuka dimbani Mei 22 katika uwanja wao wa Chamanzi Complex wakiikaribisha Mgambo JKT. Itakumbukwa kuwa Azam Fc ilishaachana na makocha wao wote waliokuja pamoja na kocha Stewart Hall na hivyo timu sasa kubaki chini ya kocha Denis Kitambi, kwani Makocha wapya waliosaini hivi karibuni wataanza majukumu ya kuiongoza Azam katika michuano ya Kagame Cup inayotarajiwa kutimua vumbi hivi karibuni.
Azam Fc Wakijiandaa na mchezo wao dhidi ya Mgambo JKT

Azam Inashika nafasi ya pili kwa kujikusanyia alama 63 huku wakiwazidi Simba inayoshika nafasi ya 3 kwa pointi 1 tu, hivyo kufanya mchezo wa mwisho kati yao na Mgambo kuwa mtihani mzito kwa kocha Kitambi kuhakikisha anaipa Azam nafasi ya pili katika ligi kuu Tanzania Bara Msimu huu kwa kushinda mechi hiyo.

Kabla ya kuwa kocha Msaidizi hapo Azam FC Kitambi alishawahi kuwa kocha mkuu baada ya aliyekuwa kocha mkuu wakati huo kutimuliwa na uongozi wa Azam na alikuja kushushwa na kuwa kocha msaidizi baada ya kuwasili kwa kocha muingereza Stewart Hall ambae ameacha kibarua hicho kwa kile alichodai amechoka kufundisha soka la Tanzania na sasa anataka kwenda kujaribu kwingine.

Related Posts:

  • YANGA SASA KUKIONA CHA MOTO Klabu ya Yanga ipo hatarini kuburuzwa katika mahakama ya kibiashara na wadhamini wao kampuni ya Bia Tanzania (TBL). Yanga Huenda ikafikishwa mahakamani kwa kile kinachodaiwa kuvunja mkataba na wadhamini wao kampuni ya TBL… Read More
  • JERRY MURO: "TFF IMETANGA VITA NA YANGA" Ofisa Habari wa Yanga, Jerry Muro amepinga vikali maamuzi ya Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF, kwa kudai kuwa haitambui adhabu hiyo na kwamba yeye ataendelea kufanya kazi. TFF imetoa adhabu ya kumfungia Jerry Mur… Read More
  • NYOTA WATATU YANGA KUKOSA MCHEZO DHIDI YA MEDEAMA Klabu ya Yanga inaendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo wa kombe la shirikisho Barani Afrika hatua ya makundi dhidi ya Medeama kutoka nchini Ghana lakini huenda wachezaji wake watatu wakaukosa mchezo huo kutokana na sababu … Read More
  • AZAM FC YAANZA KUJIWEKA FITI KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, imeanza rasmi mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya wa 2016-17. Wachezaji wa kikosi hicho wameanza kujifua wakiwa chini ya benchi jipya la ufundi linaloongozwa na makocha kut… Read More
  • SHIZA KICHUYA ATUA MSIMBAZI Klabu ya Mtibwa Sugar imethibitisha kukamilisha uhamisho wa mchezaji wao Shiza Kichuya kujiunga na klabu ya Simba. Kwa muda mrefu kichuya alikuwa akihusishwa na kujiunga na wekundu hao wa Msimbazi lakini taarifa za hivi p… Read More

0 comments:

Post a Comment