Sunday, June 19, 2016

NONGA AOMBA VILABU VIJITOKEZE KUMSAJILI

Paul Nonga ameziomba klabu ambazo zinahitaji huduma yake kufanya mazungumzo na Yanga.

Mshambuliaji huyo ambae hivi karibuni aliuandika uongozi wa Yanga barua akiwa anaomba umuuze kwenye timu nyingine kutokana na kuchoshwa na benchi, sasa amezitaka klabu zinazomhitaji zifanye mazungumzo na Yanga ili kufanikisha uhamisho wake.

Nonga hajajumuishwa katika kikosi cha Yanga kilichoenda kucheza na MO Bejaia, Algeria hivyo amesema tupo tayari hata kwa kupunguza kiasi cha mshahara ilimradi tu yeye aondoke Yanga.

"Nitafurahi kama kuna timu yoyote itajitokeza kipindi hiki tuweze kufanya biashara, nipo tayari kupunguza mshahara wangu ili timu iweze kuninunua na kuichezea msimu ujao, na najua viongozi wa Yanga ni waungwana hawatokataa ofa itakayofika mezani kwao." alisema Nonga.

Nonga alijiunga na Yanga akitokea Stand United, tangu ajiunge na Mabingwa hao wa Ligi kuu na kombe la shirikisho hajapata muda mwingi wa kucheza na hivyo kuona kila dalili za kiwango chake kupotea kwani mchezo wa soka unahitaji kucheza mara kwa mara ili uwe fiti na ujiamini unapokuwa dimbani.

Hali ya kukaa benchi imemfanya Nonga kusema yupo tayari hata kutolewa kwa mkopo kwani anachokitaka yeye ni kucheza.

Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook Hapa

Related Posts:

  • TISA WAONGEZEWA MKATABA NDANDA FC Timu ya Ndanda Fc imewaongezea mkataba wa mwaka mmoja wachezaji tisa kwa ajili ya kuendelea kukitumikia kikosi hicho msimu ujao wa Ligi Kuu Vodacom 2016/17. Msemaji wa Ndanda Fc, Idrisa Bandali aliwataja wachezaji walioon… Read More
  • RASMI: PAUL NONGA AONDOKA YANGA Aliyekuwa mchezaji wa Yanga Paul Nonga ameondoka klabuni hapo na kujiunga na klabu ya Mwadui baada ya muda mrefu kuuomba uongozi wa klabu hiyo imuuze kwenye klabu ambayo atapata nafasi ya kucheza. Paul Nonga akisaini mkata… Read More
  • MNIGERIA AHMED MUSA ATUA LEICESTER CITY Klabu ya Leicester City imemsajili mshambuliaji wa Nigeria Ahmed Musa kutoka CSKA Moscow kwa mkataba wa miaka 4 utakaogharimu pauni milioni 16. Southampton,Everton na West Ham walikuwa wakitafuta saini ya mchezaji huyo. M… Read More
  • SHIZA KICHUYA ATUA MSIMBAZI Klabu ya Mtibwa Sugar imethibitisha kukamilisha uhamisho wa mchezaji wao Shiza Kichuya kujiunga na klabu ya Simba. Kwa muda mrefu kichuya alikuwa akihusishwa na kujiunga na wekundu hao wa Msimbazi lakini taarifa za hivi p… Read More
  • PAUL POGBA AWAAGA MARAFIKI ZAKE JUVENTUS Licha ya kiwango kidogo alichoonyesha katika michuano ya Euro 2016 katika ardhi ya nyumbani, Paul Pogba anabaki akihusishwa sana na kujiunga na klabu ya Manchester United chini ya kocha Mourinho. Manchester United wanao… Read More

0 comments:

Post a Comment