Sunday, June 19, 2016

NONGA AOMBA VILABU VIJITOKEZE KUMSAJILI

Paul Nonga ameziomba klabu ambazo zinahitaji huduma yake kufanya mazungumzo na Yanga.

Mshambuliaji huyo ambae hivi karibuni aliuandika uongozi wa Yanga barua akiwa anaomba umuuze kwenye timu nyingine kutokana na kuchoshwa na benchi, sasa amezitaka klabu zinazomhitaji zifanye mazungumzo na Yanga ili kufanikisha uhamisho wake.

Nonga hajajumuishwa katika kikosi cha Yanga kilichoenda kucheza na MO Bejaia, Algeria hivyo amesema tupo tayari hata kwa kupunguza kiasi cha mshahara ilimradi tu yeye aondoke Yanga.

"Nitafurahi kama kuna timu yoyote itajitokeza kipindi hiki tuweze kufanya biashara, nipo tayari kupunguza mshahara wangu ili timu iweze kuninunua na kuichezea msimu ujao, na najua viongozi wa Yanga ni waungwana hawatokataa ofa itakayofika mezani kwao." alisema Nonga.

Nonga alijiunga na Yanga akitokea Stand United, tangu ajiunge na Mabingwa hao wa Ligi kuu na kombe la shirikisho hajapata muda mwingi wa kucheza na hivyo kuona kila dalili za kiwango chake kupotea kwani mchezo wa soka unahitaji kucheza mara kwa mara ili uwe fiti na ujiamini unapokuwa dimbani.

Hali ya kukaa benchi imemfanya Nonga kusema yupo tayari hata kutolewa kwa mkopo kwani anachokitaka yeye ni kucheza.

Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook Hapa

Related Posts:

  • Tetesi Mpya Za Usajili Liverpool Klabu ya Liverpool imefuzu kushiriki michuano ya klabu Bingwa Barani Ulaya UEFA Champions League msimu ujao wa 2017/18. Kuelekea katika michuano hiyo na ligi kuu nchini England, klabu hiyo imeshaanza kuziwania saini za wach… Read More
  • PSG Wakubali Yaishe Kwa Aubameyang Vigogo wa soka nchini Ufaransa, PSG wamekubali kutoa paundi milioni 61 kuinasa saini ya mshambuliaji wa Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang. Licha ya gharama hizo za uhamisho PSG pia wamekubali kumlipa nyota huyo kutoka b… Read More
  • Tetesi Mpya Za Usajili Arsenal Ungana na Soka24, kwa habari za papo kwa papo za usajili katika klabu kubwa na pendwa zaidi duniani, hapa nimekuwekea yanayojiri katika klabu ya Arsenal hivi sasa. Arsenal katika mbio za Kumuwania Mbappe klabu ya Arsenal… Read More
  • Tetesi Mpya Za Usajili Manchester United Tetesi za usajili katika klabu ya Manchester United. Man United Kukamilisha Uhamisho Wa Lacazette klabu ya Manchester United ipo mbioni kuhakikisha inamsajili straika wa Lyon Alexandre Lacazette, kwa mujibu wa L'Equipe … Read More
  • Yote Yanayoihusu Azam FC;Usajili, Waliotemwa Wanaoingia Na Mipango Msimu Ujao UONGOZI wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, unapenda kuwataarifu wapenzi na mashabiki wa soka nchini kuwa imebadilisha mfumo wa usajili uliokuwa ikiutumia awali wa kusajili wachezaji kwa gharama kubwa na s… Read More

0 comments:

Post a Comment