Sunday, June 19, 2016

FARID MUSSA ASUBIRI RUHUSA YA AZAM FC

Farid Mussa ni winga wa Azam FC aliyepata nafasi ya kwenda kufanya majaribio katika klabu ya Deportivo Tenerife ya nchini Hispania na kufanikiwa kufuzu majaribio hayo na sasa anasubiri ruhusa ya klabu tu ili aondoke zake.

Kiwango chake kiliwavutia viongozi wa Tenerife na kuona haja ya kuwa na winga huyo hivyo kinachosubiriwa sasa ni kukamilika kwa mazungumzo yanayoendelea baina ya klabu hizo mbili  juu ya Farid ili aweze kwenda kuanza maisha mapya katika ligi daraja la kwanza nchinni Hispania.

Farid mwenyewe amesema anaamini kwenda kwake Hispania kutasaidia kukuza kiwango chake tofauti na akibaki Tanzania.

"Ninatamani hata leo uongozi wangu unipe ruhusa kwa sababu mazingira niliyoyaona kule nilipokuwa kwenye majaribio yamenipa hamasa ya kucheza na kuamini kiwango changu kitapanda zaidi ya hapa, lakini pia kwenda kwangu Hispania kutafungua milango kwa wachezaji wengine wa kitanzania kuaminiwa na kusajiliwa huko." alisema Farid.

Safari ya Farid nchini Hispania itasaidia kuamsha hamasa kwa wachezaji wetu wa Kitanzania wanaoamini kucheza Yanga na Simba ndo mwisho wa mafanikio yao ya soka na kuwafanya waangalie mbele zaidi kwani hilo pia litasaidia kuitanganza Tanzania kimataifa na kuwa na idadi kubwa ya watanzania wanaocheza Ulaya na hatimaye kupata kikosi bora cha taifa.

Farid atakuwa Mtanzania wa pili kucheza Ulaya baada ya Mbwana Samatta anayeitumikia klabu ya KR Genk ya nchini Ubelgiji.

Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook Hapa

Related Posts:

  • SIMBA YANASA KIFAA KINGINE KIPYAKlabu ya Simba imempa mkataba wa miaka miwili kiungo Mohamed Ibrahimu tayari kwa kuitumikia klabu hiyo msimu ujao. Rais wa Simba ameyathibitisha hayo kwa kusema usajili wa Ibrahimu utasaidia kuimarisha timu yao ambayo ina … Read More
  • NONGA AOMBA VILABU VIJITOKEZE KUMSAJILIPaul Nonga ameziomba klabu ambazo zinahitaji huduma yake kufanya mazungumzo na Yanga. Mshambuliaji huyo ambae hivi karibuni aliuandika uongozi wa Yanga barua akiwa anaomba umuuze kwenye timu nyingine kutokana na kuchoshwa … Read More
  • FARID MUSSA ASUBIRI RUHUSA YA AZAM FCFarid Mussa ni winga wa Azam FC aliyepata nafasi ya kwenda kufanya majaribio katika klabu ya Deportivo Tenerife ya nchini Hispania na kufanikiwa kufuzu majaribio hayo na sasa anasubiri ruhusa ya klabu tu ili aondoke zake. … Read More
  • KIPAUMBELE NAMBA 1 CHA SIMBA KATIKA USAJILI HIKI Simba ipo katika harakati za kuimarisha kikosi chao kwa kuhakikisha hawafanyi makosa katika usajili kipindi hiki ambacho dirisha la usajili limefunguliwa. Uongozi wa Simba umesema kipaumbele chao cha kwanza katika kipindi … Read More
  • HUYU NDO ANAYETARAJIWA KUWA KOCHA MPYA SIMBABaada ya kumkosa Kalisto Pasuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Zimbabwe Simba walielekeza macho yao kwa kocha raia wa Ghana Sellas Tetteh Teivi Simba wanakaribia kumpata kocha huyo baada ya mazungumzo kwenda vizuri, Sellas… Read More

0 comments:

Post a Comment