Thursday, February 23, 2017

Kaseja mchezaji bora ligi kuu Tanzania Bara mwezi January

                                                                    kaseja

Golikipa wa timu ya Kagera sugar ya mkoani Kagera Juma Kaseja ametwaa tuzo ya mchezaji bora ya mwezi January ambayo hutolewa kila mwezi na wadhamini wa ligi hiyo kampuni ya Vodacom Tanzania.

Katika kinyang’anyiro hicho Kaseja aliwashinda Jamal S. Mtengeta wa Toto Africans ya Mwanza na Mbaraka Abeid wa Kagera Sugar.

Kaseja atakabidhiwa kitita cha shilingi milioni moja ya kitanzania na wadhamini Vodacom.

Katika mwezi January Kagera imecheza michezo mitatu na kushinda yote na kuweza kutoka nafasi ya tano hadi ya 3.


Katika michezo yote mitatu kaseja alisimama langoni na kuruhusu goli moja pekee huku Kagera wakifunga jumla ya goli 6.

0 comments:

Post a Comment