Thursday, February 23, 2017

Valencia 2 - 1 Real Madrid, Ronaldo Acharuka nusura arushe ngumi




Magoli miwili ndani ya dakika 4 yameifanya Valencia kuibuka na ushindi mbele ya vinara wa ligi kuu ya Hispania maarufu kama ’Laliga Santander’ Real Madrid .

Munir El Haddadi alipokea mpira uliokolewa na na beki wa kati wa Valencia Ezequiel Garay baada ya shambulizi kali langoni mwa Valencia. Munir El Haddadi alipiga jaro zuri na kumkuta mfungaji Simone Zaza ambae bila ajizi aliweka mpira huo wavuni.

Real Madrid wakiwa wanajiuliza wafanye nini ili warudishe goli dakika ya 9 Fabian Orellana aliipatia Valencia goli la pili kufuatia kazi nzuri ya Nani.

Madrid walionekana kupaniki baada ya goli hilo na kumshudia mchezaji bora dunia akiwa anaongea kwa hasira dhidi ya wachezaji wenzake.

Badae Madrid walirejea mchezoni na walifanikiwa kuutawala mchezo huo kwa kiwango kikubwa ndani ya kipindi cha kwanza.

Dakika ya 44 Cristiano Ronaldo aliipatia Madrid goli baada ya kazi nzuri ya beki mbrazili Marcelo.

Mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika Valencia 2 – 1 Real Madrid.

Kipindi cha pili Real Madridi walirudi na nguvu ya kutafuta magoli zaidi lakini uimara wa kulinda lango umeiwezesha timu ya Valencia kuibuka na ushindi huo.

Madrid walifanya mabadiliko kadhaa kwa lengo la kuongeza nguvu kikosi chao kwa kuwaingiza Gareth Bale 62’, Nacho Fernandez 73’ na Lucas Vazquez76’ kuchukua nafasi za James Rodriguez 62’, Raphael Varane 73’ na Luka Modric 76’

Wakati Valencia wao walifanya mabadiliko kwa lengo la kuhakikisha wanaiadhibu Madrid kwa kuwaingiza Guilherme Siqueira na kutoa Nani 39’, Carlos Soler kuchukua nafasi ya Fabian Orellana 54’ na walimtoa  Simone Zaza na kumuingiza Mario Suarez 74’.

Mabadiliko hayo yaliiwezesha  Valencia kuondoka na alama zote tatu katika dimba la Estadio Mestalla mbele ya watazamaji 45833 na kujikusanyia jumla pointi 26 baada ya michezo 23 katika nafasi ya 14.

Madrid wao wamebaki kileleni wakiwa na pointi 52 baaada ya michezo 22 wakifuatiwa kwa karibu na Barcelona wenye pointi 51 baada ya michezo 23.

Vikosi
Real Madrid:            Keylor Navas, Daniel Carvajal, Raphael Varane, Sergio Ramos, Marcelo, Luka Modric, Toni Kroos, James Rodriguez, Karim Benzema, Cristiano Ronaldo Casemiro.

Kocha:           Zinedine Zidane

Mfumo:         4:3:3

Valencia:       Diego Alves, Joao Cancelo ,Ezequiel Garay, Eliaquim Mangala, Jose Gaya, Daniel Parejo, Enzo Perez, Munir El Haddadi, Fabian Orellana, Nani, Simone Zaza

Kocha:           Voro



Mfumo:         4:2:3:1

0 comments:

Post a Comment