Saturday, May 14, 2016

SUPER MARIO AKUBALI KUJIUNGA NA MAN UNITED


Manchester United wanakaribia kumalizana na mchezaji wa Sporting Lisbon Joan Mario.
Mabosi wa United wamefanya mazungumzo mara kadhaa na mchezaji huyo mwenye miaka 23 raia wa Ureno na wakala wake anaamini dili hilo litatimia.

Mkataba wa Mario unaonyesha kuwa klabu itayohitaji kunasa saini ya mchezaji huyo inatakiwa kutoa kitita cha paundi milioni 45 na Man Utd wanaonekana  kuwa tayari kutoa kiasi hicho cha fedha na kumpa mchezaji huyo  mkataba mrefu.
Hata hivyo licha ya mkataba kuonyesha thamani ya Mario kuwa ni paundi milioni 45 Manchester watalazimika kuongeza paundi milioni 2 kutokana na mahitaji ya klabu ya Sporting.
Joan Mario

United waligeukia kwa Mario baada ya kuikosa saini ya mchezaji wa Benifica Renato Sanches ambaye amechagua kujiunga na Bayern Munich badala ya United.

Related Posts:

  • MATARAJIO YA SIMBA KIKOSI KIPYA MSIMU UJAOZacharia Hans Poppe, mwenyekiti wa kamati ya usajili Simba, amesem a kikosi chao msimu ujao kitakuwa na mabadiliko makubwa kuanzia benchi la ufundi hadi wachezaji. Simba kwa sasa ipo katika harakati za kuhakikisha wanawana… Read More
  • KIFAA KIPYA YANGA KUTUA LEO JANGWANIWalter Musona Mshambuliaji kutoka FC Platinum ya Zimbabwe anatarajiw kuwasili Daresalaam leo alasiri kwa ajili ya mazungumzo na klabu ya Yanga. Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika kutoka katika klabu ya Yanga, tayari mambo yo… Read More
  • USAJILI YANGA NI MWENDO MDUNDOKlabu ya Yanga imesema bado ina mipango ya kusajili wachezaji wa kimataifa kwa ajili ya kukisaidia kikosi chao kufanya vizuri katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika (CAF CC). Yanga imeshawanasa wachezaji wann… Read More
  • KIFAA KIPYA CHAAHIDI MAKUBWA SIMBAKiungo mshambuliaji aliyesajiliwa na Simba hivi karibuni Jamali Mnyate amesema kusaini kwake Simba mkataba wa miaka 2 ni kujiendeleza kimpira na kuisaidia Simba kupata mataji. Mnyate aliyejiunga na Simba akitokea Mwadui F… Read More
  • HUKU NDIKO SIMBA WANAKOSAKA NYOTA WAPYA Klabu ya Simba ipo katika pilikapilika za kuhakikisha wanaimarisha kikosi chao lengo likiwa ni kutwaa ubingwa wa ligi msimu ujao. Katika kuhakikisha wanafanya usajili wa uhakika Simba imeelekeza nguvu zake nchini Uganda,… Read More

0 comments:

Post a Comment