Klabu ya Yanga imesema bado ina mipango ya kusajili wachezaji wa kimataifa kwa ajili ya kukisaidia kikosi chao kufanya vizuri katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika (CAF CC).
Yanga imeshawanasa wachezaji wanne wa ndani ambao ni Hassan Ramadhani, Ben Kakolanya, Vicent Andrew na Juma Mahadhi. Habari za ndani ya Klabu ya Yanga zinasema mabingwa hao wa ligi kuu Bara wameshaanza mazungumzo na wachezaji wa kimataifa na kuna dalili za kuafikiana katika mazungumzo hayo na hayo yakishakamilika basi watawekwa hadharani.
Kwa sasa Yanga inawachezaji sita wa kigeni, Amis Tambwe, Haruna Niyonzima, Thabani Kamusoka, Donald Ngoma, Vicent Bossou na Issoufou Boubacar.
"Bado tuna nafasi ya kuongeza mchezaji na kwa sasa kuna mazungumzo yanaendelea na wachezaji kadhaa wa kimataifa, tukikubaliana wakati wowote watakuja kumalizana" alisema moja ya viongozi wa Yanga.
Kiongozi huyo alisema wakati wanaendelea na usajili huo, wanafikiria pia namna ya kulishawishi shirikisho la soka Tanzania TFF kuzidisha usajili wa wachezaji wa kigeni na kufikia kumi, lengo likiwa ni kupata nafasi ya kutafuta wachezaji wengi wazuri nje ya nchi.
Yanga itacheza mechi yake ya kwanza katika hatua ya makundi Jumapili Juni 19, dhidi ya MO Bejaia.
Bonyeza hapa ku-Like Page ya Soka24 Facebook
Wednesday, June 15, 2016
USAJILI YANGA NI MWENDO MDUNDO
Related Posts:
YAYA TOURE ASAINI MKATABA NA CAEN YA UFARANSA Ni hatua nzuri katika maisha yake ya soka, akiwa ametumikia klabu ya Aminens kwa miaka mitatu na kufanikiwa kupewa jukumu la unahodha katika kikosi cha vijana U17s, sasa hivi amepata mkataba wake mkubwa. Ikiwa… Read More
SUPER MARIO AKUBALI KUJIUNGA NA MAN UNITED Manchester United wanakaribia kumalizana na mchezaji wa Sporting Lisbon Joan Mario. Mabosi wa United wamefanya mazungumzo mara kadhaa na mchezaji huyo mwenye miaka 23 raia wa Ureno na wakala wake anaamini dili hilo li… Read More
SPURS NA ARSENAL KUWANIA SAINI YA MIDFIELD RAIA WA KENYA Tottenham Na Arsenal Wanasaka Saini Ya Midfieda Wa Southampton Victor Wanyama Wanyama alikuwa karibu kujiunga na Tottenham msimu uliopita lakini dili hilo lilifeli. Inasemekana Spurs bado wanania ya kumsajili Wanyama w… Read More
HABARI KUBWA ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO MEI 19 Arsenal Imetenga Euro Milioni 65 Kumnasa Morata Klabu ya Arsenal imetenga kitita Cha Euro Milioni 65 kuhakikisha wanapata saini ya Morata anayetumikia klabu ya Juve kwa sasa. Sessegnon & Anichebe Kuondoka West Bro… Read More
HASSAN RAMADHANI KESSY AMWAGA WINO YANGA Beki wa kulia wa Simba SC, Hassan Ramadhani Kessy (katikati) akitia dole gumba kwenye fomu za Mkataba wa Yanga, Kessy amesaini miaka miwili kuitumikia Yanga kuanzia mwezi ujao. Zoezi hilo lilifanyika juzi usiku mjini Dar… Read More
0 comments:
Post a Comment