SIMBA SC VS MWADUI FC
Simba leo wanawakaribisha Mwadui FC katika mchezo wa 27 wa
Ligi kuu Tanzania Bara, Simba wanaingia katika mechi hii wakiwa na rekodi mbaya
katika mechi za hivi karibuni, kwanii hutakiwi kukosa kuitazama mechi hii: Kocha wa
Mwadui FC, Jamhuri Kiwelu Julio amewahi kuifundisha klabu ya Simba, hivi
karibuni Julio ameutuhumu uongozi wa Simba kuwa ni wabinafsi, waroho na
wakorofi ndio kisa Simba haifanyi vizuri kwa sasa, kama hiyo haitoshi, Simba
wanaingia katika mchezo huu wakiwa katika nafasi ya 2 wakiwa na pointi 58
katika msimamo wa ligi baada ya Azam kunyang’anywa pointi tatu kwa kosa la
kumchezesha Erasto Nyoni katika mechi na Mbeya City huku akiwa ana kadi 3 za
njano, Simba wanahitaji kushinda mchezo wa leo ili kuizuia Yanga kutotangaza
ubingwa wa Ligi kuu Msimu huu mapema, lakini kinachoongeza ladha zaidi katika
mechi hii ni kauli ya Julio kocha wa Mwadui aliyosema hivi karibuni kuwa
anataka Mwadui wafanye kama walivyofanya Chelsea nchini England baada ya kutoa
sare na Tottenham na kuifananya Leicester City kuwa mabingwa wa Ligi kuu nchini
humo.
AZAM FC VS KAGERA SUGAR
Azam FC wamesafiri kuifuata Kagera Sugar katika mchezo wao
wa ligi leo, Hivi karibuni Azam FC wamepokwa pointi 3 kwa uzembe wa kumchezesha
Nyoni aliyekuwa na kadi 3 za njano, katika mchezo huu Azam FC wanahitaji
ushindi ili kurudisha matumaini kwa waajiri wao kutokana na mwenendo wao mbovu
katika ligi huku pia wakisemwa kuwa hawalipi fadhila wanazofanyiwa na waajiri
wao, ili kuleta hali ya utulivu katika klabu hiyo wanahitaji kushinda mchezo wa
leo, lakini kwa upande mwingine Kagera Sugar wao hawatakubali kufungwa kirahisi
hivyo kwani nafasi yao katika Msimamo wa ligi ni mbaya, wanashika nafasi ya 3
kutoka mwishoni wakiwa na tofauti ya pointi 2 tu na Mgambo JKT ambao wapo
katika nafasi ya kushuka Daraja, hivyo kuna kila sababu kwa Kagera Sugar kupambana
vilivyo katika mechi hii ili kujihakikishia usalama wao wa kubaki katika ligi
kuu.
0 comments:
Post a Comment