Friday, June 17, 2016

CAF YAISAFISHIA NJIA YANGA

Shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF), limemthibitisha beki Hassan Kessy kuichezea Yanga katika michuano ya Kombe la CAF CC katika hatua ya makundi.

Caf pia imetuma leseni ya wachezaji wengine watatu wa Yanga walioongezwa kwa ajili ya kushiriki michuano hiyo, ambao ni Beno Kakolanya, Juma Mahadhi na Andrew Vicent.

Hayo yamethibitishwa na Ofisa habari wa shirikisho la soka Tanzania (TFF), Alfred Licas ambaye amesema kuwa tayari leseni hizo zimetoka kwa ajili ya wachezaji hao kuanza kuitumikia klabu yao siku ya jumapili itakapocheza na MO Bejaia.

"Ni kweli tumepokea leseni za wachezaji wanne wa Yanga walioongezwa katika hatua hii, hivyo wote wapo huru kucheza michuano ya kimataifa kuanzia sasa." alisema Lucas.

Aidha kocha wa Yanga Hans Van Pluijm amesema alikuwa na kikao na wachezaji wake leo asubuhi kuwaonyesha mikanda ya video za MO Bejaia katika kubaini mapungufu yao ili wao wayatumie kupata matokeo katika mchezo wao.

"Asubuhi hii tulifanya kikkao ambapo tuliwaonyesha wachezaji wetu baadhi ya mikanda ya video ya mechi za MO Bejaia. Hivyo wanajua nini watarajie kwa wapinzani wao. " alisema Pluijm.

Yanga ilitinga hatua hii ya makundi baada ya kuiondosha Sagrada Esperanca ya nchini Angola na baadae baada ya Droo ya hatua hii kufanyika ndipo Yanga walipangwa kundi moja na timu za MO Bejaia ya Algeria, TP- Mazembe ya Congo DRC pamoja na Medeama ya nchini Ghana, na itaanza mechi yake ya kwanza dhidi ya MO Bejaia siku ya jumapili juni 19.

Related Posts:

  • RASMI: PAUL NONGA AONDOKA YANGA Aliyekuwa mchezaji wa Yanga Paul Nonga ameondoka klabuni hapo na kujiunga na klabu ya Mwadui baada ya muda mrefu kuuomba uongozi wa klabu hiyo imuuze kwenye klabu ambayo atapata nafasi ya kucheza. Paul Nonga akisaini mkata… Read More
  • MEDEAMA KUTUA DAR KESHO Wapinzani wa Yanga katika mchezo ujao wa Kombe la Shirikisho Afrika, Medeama ya Ghana wanatarajiwa kutua nchini kesho tayari kwa mchezo wa Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga katika msimamo wa Kund… Read More
  • AZAM MEDIA YAZIMWAGIA VILABU VYA VPL MAMILION Kampuni ya Azam Media imeongeza mkataba wa kurusha mechi za ligi kuu Vodacom msimu ujao 2016/17. Mkataba huo umesainiwa jana kati ya TFF na klabu ya bodi ya Ligi na Uongozi wa Azam, huku mkataba huo ukiwa umeboreshwa kido… Read More
  • HATIMAYE TFF YAMKALISHA JERRY MURO Hatimaye Ofisa Habari wa Yanga Jerry Muro, amekubali kutumikia adhabu iliyotolewa na TFF. Awali Muro alipinga adhabu hiyo kwa kutoa kauli nyingi zikionyesha kuwa TFF walikiuka taratibu za kutoa adhabu hiyo. Licha ya kauli… Read More
  • KAULI ZA WACHEZAJI YANGA KUELEKEA MECHI DHIDI YA MEDEAMA Mabingwa wa Ligi kuu Vodacom na Wawakilishi pekee Afrika Mashariki katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika klabu ya Yanga inatarajiwa kushuka dimbani kesho kumenyana na Medeama SC kutoka nchini Ghana mchezo wa tatu hat… Read More

0 comments:

Post a Comment