Harakati za usajili katika klabu ya Simba bado zinaendelea na habari za hivi karibuni zinasema makocha wanne kutoka katika nchi nne tofauti wamejitokeza kutaka kuinoa klabu hiyo.
Geofrey Nyange "Kaburu" (Makamu mwenyekiti wa klabu ya Simba) amesema kuwa kitu cha kwanza wanachokusudia kukifanya ni kuleta kocha mzungu mwenye rekodi ya kimataifa ambaye atawasaidia katika kuchagua wachezaji wa kuwasajili watakaoimarisha kikosi hicho.
Kaburu alisema hawezi kutaja nchi wanazotoka makocha hao, kikubwa ni kuwa wamevutiwa na ubora wa wasifu wao na ufahamu wao mzuri wa soka la Afrika hasa ukanda wa Afrika mashariki.
"Bado tunaendelea na mchakato wa kusaka kocha, tayari tuna maombi kutoka kwa makocha wa nchi nane tofauti, wapo wawili ambao tumevutiwa nao na tunatarajia kufanya nao mazungumzo ili kuona yupi tumchukue" alisema kaburu.
"Shida yetu kubwa ni kuiona Simba ikifanya vizuri kwenye ligi na kumaliza uteja wa kufungwa na Yanga kama ilivyokuwa msimu uliopita, ndiyo maana tukaamua kutafuta kocha mwenye kulijua vizuri soka la Afrika Mashariki na wachezaji wenyewe na tunafurahi mazungumzo yanaenda vizuri" aliongeza Kaburu.
Simba walishafanya mazungumzo na kocha Mzimbabwe Kalisto Pasuwa lakini mipango ilionekana kushindikana na kumkosa kocha huyo.
Friday, June 17, 2016
KOCHA MWENYE REKODI ZA KIMATAIFA KUTUA SIMBA
Related Posts:
PICHA ALIYOPOST MKEWE MOURINHO YAZUA UTATA UJIO WA POGBA MAN U Mashabiki wa Manchester United wamekuwa katika hali ya sintofahamu kuhusu ujio wa Pogba Man U hasa baada ya Mke wa Jose Mourinho kupost picha ambayo Mourinho amemjumuisha Pogba katika hesabu zake. Picha hiyo ilipostiwa k… Read More
YANGA WAMWONGEZEA MKATABA PLUIJM Mabingwa wa ligi kuu Vodacom na wawakilishi pekee Afrika Mashariki katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika (CAF CC), Yanga wamemwongezea mkatabawa miaka miwili kocha wao Hans Van Pluijm. Kocha huyo ambaye ame… Read More
RASMI: PAUL NONGA AONDOKA YANGA Aliyekuwa mchezaji wa Yanga Paul Nonga ameondoka klabuni hapo na kujiunga na klabu ya Mwadui baada ya muda mrefu kuuomba uongozi wa klabu hiyo imuuze kwenye klabu ambayo atapata nafasi ya kucheza. Paul Nonga akisaini mkata… Read More
SUNDERLAND YAMRUDISHA DAVID MOYES UINGEREZA Klabu ya Sunderland imemteua kocha wa zamani wa Manchester United David Moyes kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo baada ya Sam Allardyce kukabidhiwa kikosi cha timu ya taifa ya England. Moyes anachukua mikoba ya Sam Allardyce k… Read More
TAARIFA YA WAKALA WA PAUL POGBA YAZUA GUMZO Uhamisho wa Paul Pogba kwenda Manchester United umezidi kuchukua sura mpya baada ya sasa hivi kuonekana dili hilo bado kabisa kukamilika. Wakala wa Pogba, Minola Raiola, ametumia akaunti yake ya twiter kukanusa uvumi una… Read More
0 comments:
Post a Comment