Monday, May 2, 2016

JURGEN KLOPP ANASWA AKILA KILEVI

Katika ligi kuu England ni tabia mbaya kwa mchezaji kuonekana hadharani akivuta sigara, huenda labda ni kutokana na kazi yao wanayofanya ya kusakata soka ambayo inahitaji uimara wa mwili na akili pia. Na inafikia hatua makocha wa wachezaji wanaovuta sigara kuwachukulia hatua kali wachezaji hao na hata kupigwa faini wakati mwingine.
Lakini waswahili husema unapomkataza mtoto kufanya kitu ambacho wewe mwenyewe unafanya basi unapokuwa unafanya wewe jitahidi ufanyie sehemu ambapo mtoto wako hatakuona vinginevyo nae lazima atajaribu kufanya ili aone ni kwanini wewe unamkataza wakati wewe mwenyewe unafanya.


Jurgen Klopp ni kocha wa klabu ya Liverpool inayoshiriki ligi kuu nchini humo maarufu kama English Premier League, kuvuta sigara imekuwa ni tabia yake ya siku nyingi na imeonekana kuwa vigumu kwake kuiacha tabia hiyo, kocha huyo amenaswa akivuta sigara kabla ya kuenda kuongoza kikosi chake katika mazoezi. Rafiki yake wa karibu anaejulikana kwa jina la Davidi Wegner alishamzungumzia Klopp kuwa ni mvutaji mkubwa tu wa sigara, alikuwa anafanya hivyo akiwa na Mainz alifanya pia akiwa na Dortmund na anaendeleza tabia hiyo hadi hivi sasa alipojiunga na Liverpool.

Jack Wilshere ni mchezaji wa Arsenal ambae alishawahi kuingia matatani baada ya kunaswa akivuta sigara, kocha wake Arsene Wenger alilaani sana kitendo hicho.

Wachezaji wengine ambao walishawahi kunaswa wakivuta sigara ni: Wayne Rooney, Dimitar Berbatov,Fabio Coentrao, Mario Balotelli, Fabien Barthez na Kocha Carlo Ancelotti nae pia alinaswa akipitia kilevi hicho.

Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment