Monday, May 2, 2016

CLAUDIO RANIERI KAMWAMBIA MANENO HAYA VAN GAAL




Manchester United iliwakaribisha Leicester jana katika dimba la Olf Trafford, mechi ambayo Leicester City walikuwa wanahitaji kushinda ili wajitangazie ubingwa wa ligi kuu nchini humo. Lakini Man United chini ya kocha Louis Van Gaal hawakukubali vijana hao wa Ranieri wautwae ubingwa katika dimba hilo la Old Trafford kwa kutoa sare ya 1 – 1.
Kama ilivyokawaida kwa makocha kusalimiana tena baada ya mechi, ilitokea pia kwa makocha hao ambapo Claudio Ranier kocha wa Leicester City alimwambia Louis Van  Gaal kuwa anafanya kazi nzuri sana klabuni hapo licha ya watu kumsema vibaya, Van Gaal nae alimtakia kila la kheri Ranieri kwa kumwambia avute subra tu ila ubingwa ni wa kwao msimu huu.
Leicester City wanatakiwa kusubiri hadi mechi yao ijao ili endapo wakishinda watangazwe mabingwa wapya wa ligi au endapo leo Tottenham Hotspurs watafungwa na Chelsea basi Leicester watakuwa moja kwa moja mabingwa wa EPL msimu wa 2015/2016.

Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com 

0 comments:

Post a Comment