Sunday, February 19, 2017

ENGLAND: Manchester United yatinga Robo fainali FA CUP, kukutana na Chelsea robo fainali



Wakitokea benchi Zlatan Ibrahimovic na Paul Pogba dakika ya 62, waliisadia timu yao ya Manchester United kuitoa timu ya Blackburn Rovers kwa idadi ya goli 2 – 1.

Pongezi zote ziende kwa Paul Pogba ambae ndie aliefanya kazi nzuri kupitia upande wa kulia na kutoa pasi nzuri ambayo ilimaliziwa kwa ustadi mkubwa na Ibra na kuifanya united kuibuka kifua mbele.

Blackburn Rovers ndio walikuwa wa kwanza kuzifumania nyavu za United mnamo dakika ya 17 pale Daniel Graham  alipo malizia mpira kutoka kwa Marvin Emnes.
Baada ya goli hilo United walianza kulisakama lango la Rovers bila mafanikio.

Dakika ya 27 Henrik Mkhitaryan alifanya kazi kubwa na kumpa nafasi Marcus Rashford kuisawazishia United.

Mpaka mapumziko Blackburn Rovers1 – 1 Manchester United.

Kipindi cha pili dakika ya 62 Jose Mourinho aliwatoa Jesse Lingard na Anthony Martial na kuwaingiza Zlatan Ibrahimovic na Paul Pogba, mabadiliko ambayo yaliinufaisha United.

Dakika  75 Zlatan Ibrahimovic alifanya kile alichotumwa na benchi la ufundi la United baada ya kuukwamisha wavuni mpira ulitengwa na Paul Pogba .
mchezo mwingine leo ilikuwa ni kati ya Fulham waliokubali kichapo cha goli 3 kwa 

bila toka kwa Tottenham Hotspur, kwa magoli ya Harry Kane 16', 51', 73'.

Kwa Matokeo haya Manchester inaoungana na Middlesbrough, Tottenham,  Millwall, Lincoln, Chelsea katika robo fainali.

Ratiba ya Robo fainali itakuwa hivi:-

Middlesbrough vs Huddersfield/Manchester City

Tottenham vs Millwall

Chelsea vs Manchester United



Sutton /Arsenal vs Lincoln

0 comments:

Post a Comment