Monday, February 20, 2017

simba waongezewa dozi nzito Unguja


Timu ya Simba leo asubuhi imeendelea kufanya mazoezi katika Uwanja wa Amaan, simba ipo Unguja tangu ijumaa kwa maandilizi ya mchezo na mtani wake Yanga.

Simba imefikia katika Hoteli ya Mtoni Marine iliyopo Maruhubi Mkoa Mjini Magharibi, na tangu ijumaa mpaka jana ilikuwa inafanya mazoezi yake asubuhi saa 3:00 – 5:00 katika dimba la Amaan.

Mratibu wa Simba, Abbas Ally ‘Gazza’ alipohojiwa na baadhi ya waandishi wa habari wa hapa Zanzibar alisema kuhusu kufanya mazoezi asubuhi tu alisema “wanafuata Ratiba ya mwalimu na kuanzia jumatatu watakuwa wanajifua mara mbili asbubuhi na jioni katika dimba hilo”.


“simba watarejea Dar es saalam siku ya ijumaa wakiwa tayari kwa mchezo wa jumamosi” aliongeza Mratibu huyo.  

0 comments:

Post a Comment