Thursday, June 9, 2016

SAKATA LA UCHAGUZI YANGA, WAGOMBEA WAWEKEWA VIKWAZO

Wote waliochukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi Yanga kupitia TFF wametakiwa kuchua fomu upya katika makao makuu ya klabu ya Yanga.


Wagombea wote waliochukua fomu za kuwania nafasi mbalimbali za uongozi Yanga zilizotolewa na TFF wameagizwa kuchukua fomu hizo upya katika klabu ya Yanga. Mwenyekiti wa kamati ya Uchaguzi Yanga, Sam Mapande amesema wao kama kamati wamefikia uamuzi huo kwa sababu hawana uhakika kama wote waliochukua fomu hizo TFF ni wanachama halali wa Yanga.

"Hao waliochukua fomu TFF sisi hatuna uhakika kama ni wanachama wa Yanga au la, kwa hiyo wanachotakiwa ni kuomba upya, wapitie taratibu zote za kufanyiwa usaili, wakipitishwa waende kwenye uchaguzi" alisema Sam Mapande.
Hadi hivi sasa tayari wagombea wote waliochukua fomu makao makuu ya klabu ya Yanga wameshaanza kampeni takribani siku 3 zilizopita.

Wanaotakiwa kuchukua upya fomu hizo kwenye makao makuu ya timu hiyo ni;

Titus Osoro na Aaron Nyanda wanawania nafasi ya makamu mwenyekiti, Omari Said, Mchafu Ahmed Chakoma, Paschal Laizer, Edgar Chibula na Mohamed Mattaka hawa wote wanawania ujumbe wa kamati ya utendaji.

Related Posts:

  • KAPOMBE ATOA SHUKRANI ZAKE KWA MASHABIKIBAADA ya kutwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa mashabiki msimu uliopita, beki wa kulia wa Azam FC, Shomari Kapombe, amewashukuru mashabiki kwa kuonesha imani naye na kumfanya awe mshindi wa tuzo hiyo. Pia, ameeleza masikitiko ya… Read More
  • RIPOTI YA KIBADENI JKT RUVU YAANZA KUFANYIWA KAZIKocha mkuu wa JKT Ruvu Abdallah Kibadeni amewasilisha ripoti yake kwa uongozi wa timu hiyo ikiwa na mapendekezo ya wachezaji anaotaka wasajiliwe na klabu. Msemaji wa JKT Ruvu, Costantine Masanja, viongozi wa klabu hiyo tay… Read More
  • CHIRWA ATUA JANGWANI KWA SH. MILIONI 240Mshambuliaji raia wa Zambia, Obrey Chirwa amejiunga na Yanga kwa dau la sh. Milioni 240 akitokea katika klabu ya FC Platinum za Zimbabwe. Chirwa ameifungia Platinum mabao matano katika mechi nane alizocheza kwenye ligi kuu… Read More
  • RUVU SHOOTING KUKIPA NGUVU KIKOSI CHAORuvu Shooting ipo katika mipango ya kusajili wachezaji saba ili kujiimarisha kabla hawajaanza kipute cha ligi kuu Vodacom msimu wa 2016/17. kwa sasa Ruvu Shooting inaendelea na kambi kwenye uwanja wa Mabatini Mlandizi, Pwa… Read More
  • KOCHA MWENYE REKODI ZA KIMATAIFA KUTUA SIMBAHarakati za usajili katika klabu ya Simba bado zinaendelea na habari za hivi karibuni zinasema makocha wanne kutoka katika nchi nne tofauti wamejitokeza kutaka kuinoa klabu hiyo. Geofrey Nyange "Kaburu" (Makamu mwenyekiti … Read More

0 comments:

Post a Comment