Thursday, June 9, 2016

YALIYOJIRI KESI YA MWINYI KAZIMOTO

Kesi ya mchezaji wa Simba Mwinyi kazimoto kumshambulia na kumdhuru mwandishi wa habari imetolewa maamuzi yalimwacha huru mchezaji huyo .


Kesi hiyo iliyokuwa  inayomkabili mchezaji huyo wa Simba na Timu ya Taifa, Taifa Stars, ya kumshambulia mwanahabari Mwanahiba Richard imetolewa hukumu na  hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Shinyanga Rahim Mushi ambapo na huru Kazimoto baada ya kukutwa hana hatia.

Mwanahiba Richard alidai Mshitakiwa (Mwinyi Kazimoto) alimpiga makofi kwa kile alichodai kumwandia vibaya Kwenye mechi kati ya Simba na Mbeya City iliyochezwa mwaka jana.

Mwanahiba alidai mshitakiwa alimwambia hata kama atampeleka kokote hawatamfanya kitu.

Shahidi wa pili Ndg. Beni Kalama alisema wakati tukio hilo linatokea alienda kuongea na kocha wa Simba ndipo aliposikia kofi linapigwa na alipogeuka kutazama alimwona Mwanahiba akilia.

Kazimoto yeye kwa upande wake alisema alimuuliza mwandishi huyo sababu ya kumuandika vibaya kwenye gazeti lao, wakapishana kauli na ndipo Mwanahiba alipoanza kulia.

Hata hivyo mahakama imeona mchezaji Mwinyi Kazimoto hana hatia hivyo kumwachia huru.

Baada ya hukumu hiyo kusomwa Mwanahiba aliyasema haya;

""Mimi sina maamuzi yoyote, kampuni yangu ndiyo yenye mamlaka katika hili, kwahiyo labda wao ndio wanaweza kusema kama tutakata rufaa au vipi."

Related Posts:

  • MEDEAMA KUTUA DAR KESHO Wapinzani wa Yanga katika mchezo ujao wa Kombe la Shirikisho Afrika, Medeama ya Ghana wanatarajiwa kutua nchini kesho tayari kwa mchezo wa Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga katika msimamo wa Kund… Read More
  • AZAM MEDIA YAZIMWAGIA VILABU VYA VPL MAMILION Kampuni ya Azam Media imeongeza mkataba wa kurusha mechi za ligi kuu Vodacom msimu ujao 2016/17. Mkataba huo umesainiwa jana kati ya TFF na klabu ya bodi ya Ligi na Uongozi wa Azam, huku mkataba huo ukiwa umeboreshwa kido… Read More
  • JERRY MURO ATAKIWA KUWA NA ADABU Sakata la Ofisa habari wa Yanga Jerry Muro kufungiwa mwaka mmoja kutojihusisha na maswala ya soka pamoja na kupigwa faini ya sh. Milioni tatu limechukua sura mpya baada ya viongozi wa TFF kujibu kauli za Msemaji huyo. Kati… Read More
  • WANAOWANIA TUZO ZA LIGI KUU VODACOM 2015/16 Utoaji wa tuzo za washindi ligi kuu Vodacom msimu wa 2015/16 utafanyika Julai 17 jijini Dar es Salaam. Wanaowania Tuzo Hizo Ni Kama Ifuatavyo: MCHEZAJI BORA WA KIMATAIFA SH. MILIONI 5.7 Wanaowania Ni; 1. Thaban Kamusoka … Read More
  • HATIMAYE TFF YAMKALISHA JERRY MURO Hatimaye Ofisa Habari wa Yanga Jerry Muro, amekubali kutumikia adhabu iliyotolewa na TFF. Awali Muro alipinga adhabu hiyo kwa kutoa kauli nyingi zikionyesha kuwa TFF walikiuka taratibu za kutoa adhabu hiyo. Licha ya kauli… Read More

0 comments:

Post a Comment