Sunday, May 1, 2016

MAJIBU YA JUAN MATA ALIPOULIZWA KUHUSU UJIO WA MOURINHO MAN UTD


Wakati hatima ya Louis Van Gaal ikiwa haieleweki Klabuni Manchester United msimu ujao, Mourinho amekuwa akihusishwa sana na kuchukua mikoba ya Mholanzi huyo aliyebakiza mwaka mmoja klabuni hapo.
Mourinho ametokea kuwa mtu anaejadiliwa sana linapokuja suala la nani atarithi mikoba ya Van Gaal.

Kufika kwa Mourinho Chelsea kulipelekea Mata kuuzwa kutoka Chelsea na kwenda Man United Januari 2014. Hata hivyo Mhispania Mata hakupenda ku-comment chochote pale alipotakiwa kuzungumzia tetesi za ujio wa Mourihno Man United.

Mata aliiambia Daily Mail kuwa “Sidhani kama itakuwa sahihi kulizungumzia hili suala kwa sasa wakati ambapo tunae Kocha tayari, na tuna vitu vya msingi zaidi mbele yetu vya kuvifanya katika msimu huu”.

“Sio wakati sahihi kuzungumzia suala hilo” aliongeza Juan Mata ambae aliuzwa na Mourinho kutoka Chelsea.


Mata leo anatarajiwa kuungana na wachezaji wenzie kuzisaka pointi tatu ili ziwasogeze karibu na top 4 ambapo wataweza kushiriki mashindano ya UEFA Champions League msimu ujao.



Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment