Sunday, May 1, 2016

MAJIBU YA JUAN MATA ALIPOULIZWA KUHUSU UJIO WA MOURINHO MAN UTD


Wakati hatima ya Louis Van Gaal ikiwa haieleweki Klabuni Manchester United msimu ujao, Mourinho amekuwa akihusishwa sana na kuchukua mikoba ya Mholanzi huyo aliyebakiza mwaka mmoja klabuni hapo.
Mourinho ametokea kuwa mtu anaejadiliwa sana linapokuja suala la nani atarithi mikoba ya Van Gaal.

Kufika kwa Mourinho Chelsea kulipelekea Mata kuuzwa kutoka Chelsea na kwenda Man United Januari 2014. Hata hivyo Mhispania Mata hakupenda ku-comment chochote pale alipotakiwa kuzungumzia tetesi za ujio wa Mourihno Man United.

Mata aliiambia Daily Mail kuwa “Sidhani kama itakuwa sahihi kulizungumzia hili suala kwa sasa wakati ambapo tunae Kocha tayari, na tuna vitu vya msingi zaidi mbele yetu vya kuvifanya katika msimu huu”.

“Sio wakati sahihi kuzungumzia suala hilo” aliongeza Juan Mata ambae aliuzwa na Mourinho kutoka Chelsea.


Mata leo anatarajiwa kuungana na wachezaji wenzie kuzisaka pointi tatu ili ziwasogeze karibu na top 4 ambapo wataweza kushiriki mashindano ya UEFA Champions League msimu ujao.



Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

Related Posts:

  • YANGA TAYARI KWA KUIVAA MO BEJAIA Timu Ya Yanga imeshawasili nchini Algeria tayari kwa kuwavaa MO Bejaia katika mchezo wa kwanza hatua ya makundi kombe la shirikisho barani Afrika CAF CC, utakaofanyika siku ya kesho Jumapili juni 19, 2016 … Read More
  • IBRAHIMOVIC ATANGAZA KUSTAAFU SOKAZlatan Ibrahimovic 34, amesema atastaafu kuitumikia timu yake ya taifa baada ya kumalizika kwa michuano ya Euro 2016' Ibrahimovic amesema mechi yake ya mwisho ni kati ya Sweden na Ubelgiji itakayochezwa Jumatano. Sweden it… Read More
  • MEDEAMA SC KUJITOA KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA (CAF CC)Medeama huenda ikajitoa katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika CAF CC, kutokana na hali ngumu ya kifedha. Medeama imepangwa kucheza na TP-Mazembe katika mchezo wa kwanza wa hatua hiyo Juni 19,2016. CAF bado h… Read More
  • HUYU NDO KOCHA MPYA BRAZILTite ametajwa kuwa kocha mpya wa Brazil baada ya Dunga kutupiwa virago kufuatia matokeo mabovu waliyoyapata Brazil Copa America 2016. Tite Tite 55, anachukua nfasi ya Dunga aliyetimuliwa mara baada ya Brazil kutolewa hatu… Read More
  • ARGENTINA YATINGA FAINALI MESSI AWEKA REKODI COPA AMERICA Lionel Messi ameweka Rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote katika kikosi cha Argentina baada ya kufunga goli katika mechi ya robo fainali michuanoo ya Copa America dhidi ya Marekani, Mechi iliyomalizika alfajiri ya Le… Read More

0 comments:

Post a Comment