Sunday, May 1, 2016

MEMPHIS DEPAY AFUTA PICHA ZOTE ZA MAN UTD INSTAGRAM



Wakati akihusihusishwa na tetesi  za kuondoka klabuni hapo Mephis Depay amefuta picha zake zote instagram, kitu ambacho ni kama ishara tosha kuwa Mdachi huyo yupo mbioni kutimka klabuni hapo akiwa ameitumikia klabu hiyo kwa muda wa mwaka mmoja tu.

Picha zake zote alizopiga akiwa Man Utd amezifuta, huku pia akiwa ameacha kuwa-follow wachezaji wenzie wote( yani amewa-unfollow) wa klabu hiyo ya Manchester United.

Depay bado anaendelea kui-follow klabu ya Man United katika account yake ya Instagram na kwenye akaunti yake ya twitter bado ziko picha ambazo anaonekana akiwa amevaa jezi ya Man United.

Mephis Depay alisaini katika klabu ya Manchester United Msimu uliopita kwa ada ya paundi milioni 31. Tangu ajiunge na Mashetani hao winga huyo ameshindwa kuonyesha kiwango kizuri akifanikiwa kufunga magoli 2 tu katika michezo 15 aliyocheza.

Wiki chache zilizopita tetesi zilikuwa zinamhusisha Depay na kuondoka klabuni hapo baada ya  kuitumikia klabu kwa msimu mmoja tu.


Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment