Sunday, May 1, 2016

MEMPHIS DEPAY AFUTA PICHA ZOTE ZA MAN UTD INSTAGRAM



Wakati akihusihusishwa na tetesi  za kuondoka klabuni hapo Mephis Depay amefuta picha zake zote instagram, kitu ambacho ni kama ishara tosha kuwa Mdachi huyo yupo mbioni kutimka klabuni hapo akiwa ameitumikia klabu hiyo kwa muda wa mwaka mmoja tu.

Picha zake zote alizopiga akiwa Man Utd amezifuta, huku pia akiwa ameacha kuwa-follow wachezaji wenzie wote( yani amewa-unfollow) wa klabu hiyo ya Manchester United.

Depay bado anaendelea kui-follow klabu ya Man United katika account yake ya Instagram na kwenye akaunti yake ya twitter bado ziko picha ambazo anaonekana akiwa amevaa jezi ya Man United.

Mephis Depay alisaini katika klabu ya Manchester United Msimu uliopita kwa ada ya paundi milioni 31. Tangu ajiunge na Mashetani hao winga huyo ameshindwa kuonyesha kiwango kizuri akifanikiwa kufunga magoli 2 tu katika michezo 15 aliyocheza.

Wiki chache zilizopita tetesi zilikuwa zinamhusisha Depay na kuondoka klabuni hapo baada ya  kuitumikia klabu kwa msimu mmoja tu.


Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

Related Posts:

  • ANGEL DI MARIA AWEKA REKODI MPYA LIGUE 1 Mchezaji wa kimataifa wa Argentina Angel Di Maria amevunja rekodi iliyowekwa na Marvin Martin ya kutoa pasi za magoli (assists) 17 katika msimu wa 2010/11 baada ya ushindi wa magoli 4 – 0 walioupata PSG jana walipocheza … Read More
  • FAINALI UEFA CHAMPIONS LEAGUE KUAMUA HATIMA YA RONALDO MADRID Superstaa wa Real Madrid Christiano Ronaldo amekubali kubaki Real Madrid kwa Sharti moja tu. Ronaldo amesema yupo tayari kubaki Santiago Bernabeu ikiwa tu Real Madrid watafanikiwa kuifunga Atletico Madrid katika mchezo w… Read More
  • MAURICIO POCHETTINO AONGEZA MKATABA SPURS Kocha wa klabu ya Tottenham Spurs Mauricio Pochettino amesaini mkataba mpya na klabu hiyo utakaomuweka klabuni hapo hadi mwaka 2021. Pochettino alishatangaza wiki 2 nyuma kuwa alishafanya mazungumzo ya awali na klabu hiy… Read More
  • MICHEL PLATINI AJIUDHULU NAFASI YA URAIS UEFA Michel Platini jumatatu hii amejiudhulu nafasi yake ya urais katika shirikisho la mpira wa miguu barani ulaya maarufu kama UEFA, Platini amefikia hatua hiyo baada ya rufaa yake kushindikana kabisa na badala yake kupunguz… Read More
  • STRAIKA HUYU KUIHAMA BARCELONA MWISHONI MWA MSIMU Sandro Ramirez (20), alikuwa akitabiriwa kuwa ni shujaa ajae wa Barcelona. Akiwa ametokea katika Academy ya klabu hiyo ya Barcelona, lakini ameambiwa na kocha wake Luis Enrique kuwa hana mipango nae. Kwahiyo Barcelona w… Read More

0 comments:

Post a Comment