Saturday, February 11, 2017

Man U 2 - 0 Watfod, Zimebaki pointi mbili kuingia Big four



Ukiwa ni mchezo wake wa 16 mfululizo bila kupoteza katika ligi kuu ya uingereza timu ya Manchester united  imeichapa Watfod 2 – 0 na kupunguza gepu kuwania kuingia katika timu nne za juu(Big Four)

Mchezaji bora wa mchezo wa leo Anthony Martial alimtengenezea nafasi kiungo mtafutaji Juan Mata 32’ na Mata akaukwamisha mpira wavuni na kuwaamsha Washabiki waliojaa katika majukwaa ya Old Trafford.

                                                                     Juan Mata 

60’ Anthony Martial alimalizia kazi nzuri iliyofanywa na mkongwe Zlatan Ibrahimovic na kuiandika UTD goli la pili.
                                                              Anthony Martial

Mchezo wa  leo nusura uishe bila kadi yoyote lakini Antonio Valencia alipewa kadi ya njano 90’.

Hadi mpira unamalizika UTD 2 – 0 Watfod, baada ya mchezo huo UTD wamefikisha point 48, point 2 nyuma ya Tottenham na Arsenal wanaoshika nafasi ya 2 n 3.

Pamoja na ushidi huo bado Man U wanabaki katika nafasi yao ya 6 ambayo imekuwa ni ngumu kwao kuikimbia kwa muda mrefu sasa.

Matokeo mengine ni kama yanavyoonekana
 Middlesbrough 0 - 0 Everton
West Ham United 2 - 2 West Bromwich Albion
Sunderland 0 - 4 Southampton
Stoke City 1 - 0 Crystal Palace

0 comments:

Post a Comment