Sunday, February 12, 2017

Sadio Mane aitungua Tottenham bila huruma, Liverpool 2 - 0 Tottenham



Magoli mawili ndani ya dakika mbili yaliyofungwa na Msenegali Sadio Mane yameiwezesha Liverpool kufikisha point 49 nyuma ya Chelsea yenye 59, Tottenham na Arsenal zote zikiwa na 50 kila moja.

Dakika ya 16 Georginio Wijnaldum alimtengenezea nafasi Sadio Mane nae bila ajizi akaukwamisha mpira kwenye goli la Tottenham .

18’ Sadio Mane tena alijetenga na kumalizia mpira uliookolewa na kipa wa Tottenham baada ya shuti kali la Adam Lallana na kuipa Liverpool uongozi wa 2 – 0 mpka mapumziko.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi Tottenham wakijaribu kukomboa na Liverpool wakijaribu kuongeza lakini mpaka 90’ Matokeo yakabaki Liverpool 2 – 0 Tottenham.

Wachezaji watano wa Tottenham walionyeshwa kadi za njano ambao ni: Heung-Min Son 28’, Harry Kane 67’, Harry Winks 71’, Eric Dier 78’ na Toby Alderweireld 83’

Wachezaji watatu wa Liverpool nao walionywa kwa kadi za njano:  Jordan Henderson 53’, Joel Matip 56’, James Milner 68’.

Vikosi
Liverpool :
Simon Mignolet, Nathaniel Clyne, James Milner, Lucas Leiva(82’), Joel Matip, Adam Lallana, Jordan Henderson, Georginio Wijnaldum, Sadio Mane(90’), Roberto Firmino, Philippe Coutinho 77’
substitutions:
Emre Can 77’, Ragnar Klavan 82’, Trent Alexander-Arnold 90’ Loris Karius, Daniel Sturridge, Alberto Moreno, Divock Origi

Kocha:      Jurgen Klopp

Tottenham :
Hugo Lloris, Kyle Walker, Ben Davies, Toby Alderweireld, Eric Dier, Victor Wanyama, Moussa Dembele77’, Christian Eriksen 68’, Dele Alli, Heung-Min Son 82’, Harry Kane

substitutions:
Harry Winks 68’, Moussa Sissoko 77’, Vincent Janssen 82’, Georges N'Koudou, Kieran Trippier, Kevin Wimmer


Kocha:    Mauricio Pochettino

0 comments:

Post a Comment