Tuesday, November 8, 2016

Huzuni yatanda Tanzania baada kuondokewa na Mzee Said Mohamed Abeid


Majonzi yametawala katika nyuso za wapenda soka nchini baada ya kuondokewa na Mzee Said Mohamed Abeid ambae ni mwenyekiti wa timu ya Azam pia ni makamu mwenyekiti wa bodi ya ligi kuu Tanzania bara na mjumbe wa kamati mbalimbali za shirikisho la soka Tanzania, TFF.
Mpaka umauti unamkuta alasir ya jana Novemba 7, 2016, na Mzee Said Mohamed Abeid alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Aga Khan ya jijini Dar es Salaam.
Huko shinyanga ambapo timu ya Azam imekwenda kumalizia mchezo wake wa mwisho dhidi ya Mwadui FC hali ya huzuni imetanda sana Miongoni mwa wachezaji, benchi la ufundi, na viongozi wote walioambata na timu hiyo
Mzee Said atakumbukwa Kutokana na mchango wake mkubwa katika kilabu ya Azam tangu kupanda daraja miaka 8 iliyopita, chini ya uongozi wake Azam imeweza kutwaa makombe mbalimbali ikiwemo ligi kuu Tanzania Bara, Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, mapinduzi cup.
Mzee Saidi atakumbukwa kwa uchesi,upendo, ukarimu na uchapakazi wake katika soka la Tanzania.
Marehem alizaliwa visiwani Zanzibar mnamo tarehe 20 Machi 1940, amezikwa leo Jumanne ya tarehe 8 Novemba, 2016 kwenye makaburi ya Kisutu baada ya swala ya saa kumi (Alasir).

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu Mzee Said Mohamed Abeid mahali pema peponi amiin

Related Posts:

  • KAULI YA FARID MUSSA BAADA YA KUTUA NCHINI Farid Mussa, amesema kuwa hivi sasa yupo fiti kukabiliana na changamoto ya soka la Hispania endapo atajiunga na Club Deportivo Tenerife msimu ujao. Farid aliyerejea nchini jana akitokea katika timu hiyo inayoshiriki Li… Read More
  • HIZI NDO MECHI ZOTE ZA KUFUNGA LIGI LEO Ligi kuu Tanzania Bara Maarufu Vodacom ijatarajiwa kuendelea tena leo kwa mechi za mwisho za kufunga pazia la ligi hiyo. Michezo itakayopigwa leo ni pamoja na Simba itakayokipiga na JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar… Read More
  • YUSUFU MANJI AWAPA MAGARI WACHEZAJI YANGA Mwenyekiti wa klabu ya Yanga Yusufu Manji ameahidi kuwapa magari wachezaji wa timu hiyo baada ya kufanikiwa kutinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika CAF, baada ya kuiondosha  Sagrada Esperanca ya Angola. … Read More
  • PAZIA LA LIGI KUU VODACOM KUFUNGWA RASMI KESHO Michezo ya mwisho ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, inatarajiwa kufanyika kesho Jumapili, Mei 22, 2016 kwa timu zote 16 kutinga katika viwanja vinane tofauti kumaliza ngwe ya msimu wa 2015/16. Michezo itakayopigwa … Read More
  • WANAOSUGUA BENCHI YANGA KUCHEZA NA MAJIMAJI LEO Yanga imewasili Mjini Songea tayari kuvaana na Majimaji katika mchezo wao wa mwisho wa Ligi kuu Tanzania Bara. Kuelekea mchezo huo Yanga imepeleka kikosi ambacho wengi wa wachezaji wake hawapati muda mwingi wa kucheza uk… Read More

0 comments:

Post a Comment