Saturday, May 21, 2016

KAULI YA FARID MUSSA BAADA YA KUTUA NCHINI

Farid Mussa, amesema kuwa hivi sasa yupo fiti kukabiliana na changamoto ya soka la Hispania endapo atajiunga na Club Deportivo Tenerife msimu ujao.





Farid aliyerejea nchini jana akitokea katika timu hiyo inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza Hispania ‘Segunda Division’, amefuzu majaribio kujiunga na timu hiyo na kinachosubiriwa hivi sasa ni kumalizika kwa mazungumzo baina ya viongozi wa Azam FC na timu hiyo iliyoonyesha nia kubwa ya kumsajili winga huyo baada ya kuridhishwa naye kwa kipindi cha mwezi mmoja alichotumia kwa majaribio hayo.

Farid amesema kuwa amekutana na changamoto nyingi sana alipokuwa kwenye majaribio ndani ya kikosi hicho hadi kufuzu, lakini hivi sasa ameshazizoea na yupo tayari kwa mapambano endapo atajiunga nayo kwa msimu ujao.

“Kwanza kule nimekutana na hali ya hewa na mandhari tofauti na hapa, pia vyakula navyo ni tofauti sana hivyo ilinichukua muda kuzoea mambo yote hayo, hata mfumo wa uchezaji na mazoezi ya wenzetu ni tofauti sana, mwanzo ilinipa shida sana lakini hivi sasa nimezoea na kuona ni kawaida sana.

“Hata wenyewe walinishangaa sana kwa namna nilivyozoea haraka na nilivyokuwa nacheza, naweza kusema nipo fiti hivi sasa kupambana na changamoto zote kule,” alisema.

“Najisikia vizuri sana kufuzu majaribio na namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa hatua niliyofika, watu wa kule Hispania wameonyesha kunikubali sana na najivunia kwa hilo kiukweli nimefurahishwa na hilo sana, kwa hiyo mimi ni juhudi tu nitakazoziongeza kwenye mazoezi kwani malengo ninayoyataka mimi na sehemu ninayotaka nifike bado sana na ndio maana napambana sana niwezavyo,” alimalizia.

Farid aliyekuzwa kwenye kituo cha kulelea vipaji cha Azam FC ‘Azam FC Academy’, hadi anapata nafasi hiyo ya kwenda Hispania kwa kiasi fulani imechangiwa na kiwango chake bora msimu huu baada ya kuchezeshwa mara kwa mara katika kikosi cha timu kubwa.

Related Posts:

  • KIKOSI CHA SIMBA CHAPEWA LIKIZO FUPI SIMBA iliyotoka kucheza na Mtibwa Sugar jana na kuibuka na ushindi wa goli moja kwa bila goli lililofungwa na Abdi Banda, imepewa mapumziko mafupi kabla ya kuanza kujiandaa na mchezo wao wa mwisho wa ligi dhidi ya JKT Ru… Read More
  • STEWART HALL APEWA MKONO WA KWAHERI AZAM FC KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, leo imeachana rasmi na aliyekuwa Kocha Mkuu wake, Stewart Hall, baada ya kufanyika makubaliano ya pande zote mbili. Uongozi wa Azam FC inayodhaminiwa na Benki ya NMB,… Read More
  • TFF YABEBESHWA LAWAMA MATOKEO MABAYA YA SIMBA SC RAIS wa Simba Sports Club Evans Aveva jana alijitokeza mbele ya waandishi wa habari akielezea hali mzima ya ligi kuu Tanzania Bara na muendelezo wa matokeo mabaya ya Simba. Katika hotuba yake Aveva ameitupia lawama TFF … Read More
  • HIZI NDO ZITAKAZOSHUKA DARAJA LIGI KUU BARA Wakati Coastal Union ya Tanga ikiwa imeaga rasmi Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania 2015/16, swali linabaki kwa wadau wa soka nchini kwamba ni timu gani itaungana na Wagosi wa Kaya kushuka daraja kutokana na timu tano kuwa kat… Read More
  • SERENGETI BOYS YAGAWA DOZI INDIA Timu ya soka ya Taifa ya Vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ leo Mei 17, 2016 imechanua vema baada ya kuilaza India mabao 3-1 katika mchezo wake wa pili wa michuano maalumu ya kimataifa iliyoandaliwa… Read More

0 comments:

Post a Comment