Saturday, May 14, 2016

NDANDA FC WAPANIA KUHARIBU SHEREHE YA YANGA


Msemaji wa klabu ya Ndanda FC Idrisa Bandari amesema watahakikisha wanaifunga Yanga na kuharibu Sherehe yao ya kukabidhiwa kombe leo katika mchezo utakaopigwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar.
Yanga wanaingia katika mchezo wa leo wakiwa tayari mabingwa huku mchezo huo ukiambatana na sherehe za kukabidhiwa kombe la ligi kuu Bara msimu wa 2015/16, 

Bandari amesema kwao wao mchezo wa leo una umuhimu mkubwa huku wakitaka kutoka katika nafasi waliyopo katika msimamo wa ligi na kusogea katika nafasi za juu zaidi, akizungumza jana Idrisa amedai kikosi cha Ndanda kimejiandaa vizuri na kipo tayari kuwavaa Mabingwa hao wa ligi kuu Tanzania Bara mara 26.

Kwa upande mwingine afisa habari wa Yanga, Jerry Muro amesema wao hawauchukulii mchezo huo kama bonanza bali mchezo ambao wanahitaji kushinda ili kuweka heshima zaidi katika ligi kuu Bara, akizungumza kwa majigambo Muro amesema Yanga ni Wakimataifa na wanataka kulithibitisha hilo pia kwa kushinda mechi ya leo, aliendelea kwa kusema sio ajabu kwa mashabiki watakao hudhuria leo uwanjani wakamuona Donald Ngoma akikaa golini badala ya kucheza ndani huku Ally Mustafa na Deogratius Munish wakicheza ndani kwani wote ni wachezaji na ni katika kuuthibitishia umma kuwa Yanga inaweza na kwamba inaweza pia kufanya kitu chochote katika mpira.

Tayari TFF wameshatangaza kuwa Waziri wa Kilimo, Ufugaji na Uvuvi Mwigulu Nchema ndiye atakaekabidhi kombe hilo kwa vijana wa Jangwani katika sherehe hizo zitakazofanyika baada ya mechi kumalizika, Yanga pia wanatarajia kusafiri kwenda Angola kucheza mechi ya marudiano hatua ya mtoano kombe la shirikisho barani Afrika dhidi ya GD Sagrada Esperanca.

Related Posts:

  • RATIBA LIGI KUU BARA LEO JUMAPILI Michezo kadhaa kupigwa jumapili hii kote duniani tukianzia nyumbani Tanzania ligi kuu Tanzania Bara kuendelea katika viwanja vinne vya miji tofauti. Macho ya wapenda michezo wengi Afrika mashariki yapo uwanja wa Uhuru a… Read More
  • BAADA YA KUZUILIWA TAIFA, YANGA KUCHEZA HAPA Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) inatarajiwa kuendelea keshokutwa Jumatano Oktoba 12, 2016 kwa michezo saba huku ule mchezo kati ya Young Africans ya Dar es Salaam dhidi ya Mtibwa Sugar ya Morogoro ukipangwa kufanyika… Read More
  • MATOKEO LIGI KUU BARA LEO SIMBA YATAKATA UHURU Simba imeendeleza wimbi lake la ushindi msimu huu baada ya  leo kuifunga timu ngumu ya kagera sugar ya mkoani kagera katika mchezo ulichezwa uwanja wa Uhuru jiji Dar es salaam, na hii inamainisha samba imeshinda mch… Read More
  • MATOKEO YA MICHEZO YA LEO VPL MATOKEO YA MICHEZO YA LEO VPL Uwanja wa uhuru tumeshuhudia mpira ukiwa ni wa kupaniana sana hasa kipindi cha kwanza ambapo kadi za njano nyingi zilitoka na huku kila timu ikionekana kutokumwamini mwamuzi Israel Nkongo. … Read More
  • Hans Van Pluijm arejea jangwani asimamia mazoezi jioni ya leo Hatimae mwigulu Nchemba amrejesha tena kundini kocha mkuu wa yanga Hans Van Pluijm na join hii amekiongoza kikosi cha yanga katika mazoezi yakujiandaa na mchezo wa wikiendi hii na Mbao FC. Mwigulu ambae ni waziri kati… Read More

0 comments:

Post a Comment