Sunday, October 16, 2016

RATIBA LIGI KUU BARA LEO JUMAPILI


Michezo kadhaa kupigwa jumapili hii kote duniani tukianzia nyumbani Tanzania ligi kuu Tanzania Bara kuendelea katika viwanja vinne vya miji tofauti.
Macho ya wapenda michezo wengi Afrika mashariki yapo uwanja wa Uhuru ambapo utafanyika mchezo namba 76 utakao zikutanisha Azam matajiri hawa wa jiji na mabingwa watetezi wa ligi hiyo Yanga, ikumbukwe kua Yanga na Azam  wanapokutana Hakuna kuoneana haya kwani hua huwezi kutabiri ni nani ataibuka mshindi wa mchezo. Mchezo huo wa leo jioni majira ya saa kumi utachezeshwa na mwamuzi  Israel Nkongo wa Dar es Salaam. Nkongo atasaidiwa na Soud Lila na Frank Komba na mwamuzi wa akiba atakuwa Helen Mduma; wote wa Dar es Salaam. Kamishna wa mchezo atakuwa Michael Wambura pia wa Dar es Salaam.
Mchezo mwingine ni mchezo namba 77 utakaopigwa dimba la Mabatini Mlandizi Pwani wakati wenyeji Ruvu Shooting ya Pwani zidi ya timu ya jiji la Mbeya Mbeya city mchezo utakaochezeshwa na mwamuzi  Rudovic Charles wa Tabora akisaidiwa na Samwel Mpenzu wa Arusha na Jeremina Simon wa Dar es Salaam.Kamisha wa mchezo huo atakuwa Idelfonce Magali wa Morogoro.
Mchezo mwingine utazikutanisha Mtibwa sugar ambayo inakumbukumbu ya kipigo cha goli 3 kwa 1 kutoka kwa Yanga katikati ya wiki wataikaribisha Tanzania Prisons ya Mbeya katika mchezo namba 78 ambao utachezeshwa na mwamuzi  Elly Sasii wa Dar es Salaam. Waamuzi wasaidizi ni Ferdinand Chacha wa Mwanza Lulu Mushi wa Dar s Salaam wakati mwamuzi wa akiba Nicolaus Makalanga wa Morogoro. Kamishna ni George Komba wa Dodoma.
Mchezo mwingine ni ule wenye namba 78 kati ya wenyeji wa mkoa wa mwanzaToto African ya Majimaji ya Songea kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mchezo huo utasimamiwa na mwamuzi Shomary Lawi wa Kagera akisaidiwa na Abdallah Uhako wa Arusha na Julius Kasitu wa Shinyanga huku mwamuzi wa akiba akiwa Mathew Akrama wa Mwanza. Kamishna atakuwa Michael Bundala wa Dar es Salaam.
Ratiba hii ni kwa msaada wa Tff
Michezo yote itapigwa saa kumi kamili jioni





Related Posts:

  • KAPOMBE ATOA SHUKRANI ZAKE KWA MASHABIKIBAADA ya kutwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa mashabiki msimu uliopita, beki wa kulia wa Azam FC, Shomari Kapombe, amewashukuru mashabiki kwa kuonesha imani naye na kumfanya awe mshindi wa tuzo hiyo. Pia, ameeleza masikitiko ya… Read More
  • RIPOTI YA KIBADENI JKT RUVU YAANZA KUFANYIWA KAZIKocha mkuu wa JKT Ruvu Abdallah Kibadeni amewasilisha ripoti yake kwa uongozi wa timu hiyo ikiwa na mapendekezo ya wachezaji anaotaka wasajiliwe na klabu. Msemaji wa JKT Ruvu, Costantine Masanja, viongozi wa klabu hiyo tay… Read More
  • FARID MUSSA ASUBIRI RUHUSA YA AZAM FCFarid Mussa ni winga wa Azam FC aliyepata nafasi ya kwenda kufanya majaribio katika klabu ya Deportivo Tenerife ya nchini Hispania na kufanikiwa kufuzu majaribio hayo na sasa anasubiri ruhusa ya klabu tu ili aondoke zake. … Read More
  • KIPAUMBELE NAMBA 1 CHA SIMBA KATIKA USAJILI HIKI Simba ipo katika harakati za kuimarisha kikosi chao kwa kuhakikisha hawafanyi makosa katika usajili kipindi hiki ambacho dirisha la usajili limefunguliwa. Uongozi wa Simba umesema kipaumbele chao cha kwanza katika kipindi … Read More
  • BOCCO ATAJA KILICHOWAPONZA AZAM FCNahodha wa timu ya Azam FC, John Bocco amesema kuwa kushindwa kupata mafanikio katika msimu uliopita kumechangiwa na kuwakosa wachezaji wao muhimu katika kikosi hicho. Bocco alisema kukosekana kwa wachezaji muhimu katika k… Read More

0 comments:

Post a Comment