Sunday, May 8, 2016

MASHABIKI WAMPA MKONO WA KWAHERI NYOTA HUYU ANAEJIUNGA NA LIVERPOOL



Mchezaji wa kimataifa wa Cameroon Matip (24) ameichezea klabu ya Schalke 04 katika maisha yake yote ya soka hadi sasa, amecheza michezo 260 katika klabu katika mashindano yote tangu aanze kucheza klabuni hapo mwaka 2009.

Kabla ya mechi yao waliyocheza katika uwanja wao wa nyumbani dhidi ya Augsburg, mashabiki wa Schalke 04 walitandaza bango kubwa nyuma ya lango moja la goli likiwa na ujumbe uliotafsiriwa kuwa “Kwa miaka 16 umejitolea kila kitu chako kwa ajili ya Schalke-Asante sana Jimmy”

Matip amefunga magoli 3 katika ligi msimu huu. Ni mchezaji kipenzi cha mashabiki wa Schalke na itakuwa vigumu kuziba pengo lake kwani amekuwa na kiwango kizuri sana katika mechi zote za ligi alizocheza.

Mwisho wa Msimu huu Matip anatarajia kujiunga na Klabu ya Liverpool, ikiwa tayari ameshasaini makubaliano ya awali na klabu hiyo ya Liverpool.

0 comments:

Post a Comment