Wednesday, June 22, 2016

KIMESHAELEWEKA YANGA WAPYA WOTE RUKSA ISIPOKUWA HUYU

Wachezaji wote wapya wa Yanga wamethibitishwa kuwa huru kuanza kuitumikia klabu hiyo isipokuwa Hassan Ramadhan Kessy.

Yanga imewasajili wachezaji watano hadi sasa ambao ni Andrew Vicent, Juma Mahadhi, Ben Kakolanya, Hassan Ramadhan pamoja na Obrey Chilwa. Katika wachezaji hao ni Hassan Ramadhan tu ambaye bado taratibu zake za uhamisho hazijakamilika baada ya Simba kukataa kuwaandikia barua Yanga kumruhusu mchezaji huyo kuanza kuitumikia Yanga.

Hata hivyo klabu ya Yanga imewaandikia barua Simba SC kuwauliza kama kuna pingamizi lolote juu ya mchezaji huyo huku wakiambatanisha na mkataba wa Kessy unaoonyesha kumalizika Juni 15 na kwamba endapo Simba hawatojibu barua hiyo basi watachukua hatua ya kulipeleka suala hilo TFF ili waweze kulitolea maamuzi.

Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook Hapa

Related Posts:

  • YANGA WAMWONGEZEA MKATABA PLUIJM Mabingwa wa ligi kuu Vodacom na wawakilishi pekee Afrika Mashariki katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika (CAF CC), Yanga wamemwongezea mkatabawa miaka miwili kocha wao Hans Van Pluijm. Kocha huyo ambaye ame… Read More
  • PICHA ALIYOPOST MKEWE MOURINHO YAZUA UTATA UJIO WA POGBA MAN U Mashabiki wa Manchester United wamekuwa katika hali ya sintofahamu kuhusu ujio wa Pogba Man U hasa baada ya Mke wa Jose Mourinho kupost picha ambayo Mourinho amemjumuisha Pogba katika hesabu zake. Picha hiyo ilipostiwa k… Read More
  • RASMI: PAUL NONGA AONDOKA YANGA Aliyekuwa mchezaji wa Yanga Paul Nonga ameondoka klabuni hapo na kujiunga na klabu ya Mwadui baada ya muda mrefu kuuomba uongozi wa klabu hiyo imuuze kwenye klabu ambayo atapata nafasi ya kucheza. Paul Nonga akisaini mkata… Read More
  • SUNDERLAND YAMRUDISHA DAVID MOYES UINGEREZA Klabu ya Sunderland imemteua kocha wa zamani wa Manchester United David Moyes kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo baada ya Sam Allardyce kukabidhiwa kikosi cha timu ya taifa ya England. Moyes anachukua mikoba ya Sam Allardyce k… Read More
  • TAARIFA YA WAKALA WA PAUL POGBA YAZUA GUMZO Uhamisho wa Paul Pogba kwenda Manchester United umezidi kuchukua sura mpya baada ya sasa hivi kuonekana dili hilo bado kabisa kukamilika. Wakala wa Pogba, Minola Raiola, ametumia akaunti yake ya twiter kukanusa uvumi una… Read More

0 comments:

Post a Comment