Sunday, May 15, 2016

ANGEL DI MARIA AWEKA REKODI MPYA LIGUE 1


Mchezaji wa kimataifa wa Argentina Angel Di Maria amevunja rekodi iliyowekwa na Marvin Martin ya kutoa pasi za magoli (assists) 17 katika msimu wa 2010/11 baada ya ushindi wa magoli 4 – 0 walioupata PSG jana walipocheza na Nantes.

Di Maria amevunja rekodi hiyo kwa kufikisha pasi za magoli (assists) 18 katika msimu uliomalizika hivi punde wa 2015/16.

Katika mchezo wa wao dhidi ya Nantes Di Maria alitoa pasi zilizozaa magoli akimpasia Zlatan Ibrahimovic na Lucas Moura katika ushindi huo wa 4 – 0.

Rekodi iliyovunjwa ya assists 17 iliwekwa na Marvin Martin akiwa na FC Sochaux’s msimu wa 2010/11

0 comments:

Post a Comment