Sunday, May 1, 2016

DI MARIA NA IBRAHIMOVIC WANG'AA WAKATI PSG IKIIADHIBU RENNES



VIGOGO wa ligi ya Ufaransa Ligue 1, wameendeleza ubabe wao tena jana kwa kuishushia kichapo kikali cha magoli 4 - 0 timu ya Rennes, mchezo uliopigwa katika dimba linalomilikiwa na Paris Saint-Germain, Parc des Princes.

Di Maria na Ibrahimovic walionyesha kiwango bora katika mchezo huo, huku Ibrahimovic akifanikiwa kufunga magoli mawili dakika ya 54 na 78.
Magoli mengine ya PSG yalifungwa na Maxwell 50' na la 4 lilifungwa na Cavani dakika za nyongeza za mchezo.

Matokeo hayo yameifanya PSG kufikisha pointi 89 katika michezo 35, wakishika nafasi ya kwanza huku wakifuatiwa kwa mbali na Olympique Lyonnais waliojikusanyia pointi 69 katika nafasi ya pili huku wakiwa wameshacheza michezo 36.




Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

Related Posts:

  • YAYA TOURE ASAINI MKATABA NA CAEN YA UFARANSA Ni hatua nzuri katika maisha yake ya soka, akiwa ametumikia klabu ya Aminens kwa miaka mitatu na kufanikiwa kupewa jukumu la unahodha katika kikosi cha vijana U17s, sasa  hivi amepata mkataba wake mkubwa. Ikiwa… Read More
  • DI MARIA NA IBRAHIMOVIC WANG'AA WAKATI PSG IKIIADHIBU RENNES VIGOGO wa ligi ya Ufaransa Ligue 1, wameendeleza ubabe wao tena jana kwa kuishushia kichapo kikali cha magoli 4 - 0 timu ya Rennes, mchezo uliopigwa katika dimba linalomilikiwa na Paris Saint-Germain, Parc des Princes… Read More
  • ANGEL DI MARIA AWEKA REKODI MPYA LIGUE 1 Mchezaji wa kimataifa wa Argentina Angel Di Maria amevunja rekodi iliyowekwa na Marvin Martin ya kutoa pasi za magoli (assists) 17 katika msimu wa 2010/11 baada ya ushindi wa magoli 4 – 0 walioupata PSG jana walipocheza … Read More
  • ZLATAN IBRAHIMOVIC ATANGAZA RASMI KUONDOKA PSG Paris: Zlatan Ibrahimovic amethibitisha ijumaa hii kuwa ataihama klabu ya Paris Saint-Germain mwishoni mwa msimu huu wa ligi, lakini Uongozi wa mabingwa hao wa ligi kuu nchini Ufaransa ligue 1 wamesema nyota huyo atarudi… Read More
  • Christiano Ronaldo Kutua PSG France football imetoa habari iliyotikisa zaidi kwa wapenzi wa soka ikimhusisha Star wa Real Madrid Christiano Ronaldo kutua katika klabu ya PSG. Habari kutoka chanzo hicho zinaripoti kuwa Ronaldo amekutana mara 5 na Rai… Read More

0 comments:

Post a Comment