Wednesday, June 8, 2016

BEKI WA BLACK LEOPARDS YA AFRIKA KUSINI KUTUA SIMBA

Mwenyekiti wa kamati ya usajili Simba Hans Poppe yupo katika mazungumzo na Beki wa kati wa klabu ya Black leopards ya nchini Afrika kusini Harry Nyirenda.


Hans Pope yupo nchini Zimbabwe kukamilisha usajili wa kocha Kalisto Pasuwa sambamba na kufanya mazungumzo na beki wa kati anayecheza katika klabu ya Black Leopards ya nchini Afrika kusini.

Harry Nyirenda raia wa Malawi ameonyesha kiwango kizuri kilichomvutia Hans Pope wakati timu yake ya taifa ya Malawi ilipocheza na Zimbabwe na hivyo kumuona kuwa ni mbadala mzuri wa Juuko Murshid aliyetimka katika kikosi cha Simba.



"Nimevutiwa na uwezo wake akiwa na timu ya taifa ya Malawi ilipocheza na Zimbabwe, nadhani anaweza kuwa msaada mkubwa kwetu kama tutafanikiwa kumpata ili kusaidiana na Novaty Lufungo" alisema Hans Pope alipozungumza na Goal.

Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo tayari wameshaanza mazungumzo na beki huyo na kama mambo yataenda sawa basi moja kwa moja mashabiki wa Simba watashuhudia beki huyo akitua katika klabu yao.

0 comments:

Post a Comment