Wednesday, June 8, 2016

BEKI WA BLACK LEOPARDS YA AFRIKA KUSINI KUTUA SIMBA

Mwenyekiti wa kamati ya usajili Simba Hans Poppe yupo katika mazungumzo na Beki wa kati wa klabu ya Black leopards ya nchini Afrika kusini Harry Nyirenda.


Hans Pope yupo nchini Zimbabwe kukamilisha usajili wa kocha Kalisto Pasuwa sambamba na kufanya mazungumzo na beki wa kati anayecheza katika klabu ya Black Leopards ya nchini Afrika kusini.

Harry Nyirenda raia wa Malawi ameonyesha kiwango kizuri kilichomvutia Hans Pope wakati timu yake ya taifa ya Malawi ilipocheza na Zimbabwe na hivyo kumuona kuwa ni mbadala mzuri wa Juuko Murshid aliyetimka katika kikosi cha Simba.



"Nimevutiwa na uwezo wake akiwa na timu ya taifa ya Malawi ilipocheza na Zimbabwe, nadhani anaweza kuwa msaada mkubwa kwetu kama tutafanikiwa kumpata ili kusaidiana na Novaty Lufungo" alisema Hans Pope alipozungumza na Goal.

Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo tayari wameshaanza mazungumzo na beki huyo na kama mambo yataenda sawa basi moja kwa moja mashabiki wa Simba watashuhudia beki huyo akitua katika klabu yao.

Related Posts:

  • KIBARUA CHA LAURENT BLANC CHAOTA NYASI PSGKlabu ya PSG imemtimua kocha wake Laurent Blanc, kwa mujibu wa jarida la la L'Equipe la nchini Ufaransa. Taarifa za kutimuliwa kwa kocha huyo bado hazijawa rasmi kwani mpaka hivi sasa klabu ya PSG haijatoa tamko rasmi laki… Read More
  • MOURINHO AKERWA NA MAAMUZI YA ED WOODWARDKocha mpya wa Man U Jose Mourinho amekerwa na kitendo cha bosi wake Ed Woodward kushindwa kukamilisha dili la Renato Sanches. United tayari imeshakamilisha usajili wa mlinzi kutoka Villarreal, Eric Bailly kwa uhamisho wa p… Read More
  • RASMI:DANI ALVES ATUA JUVENTUSMchezaji wa kimataifa wa Brazil, Dani Alves ametua katika klabu ya Juventus akitokea Barcelona. Dani Alves amekamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Juventus akitokea Barcelona na kusaini mkataba wa miaka miwili na mabingw… Read More
  • SIMBA YAITOLEA NJE YANGAKlabu ya Simba imekanusha taarifa zilizotolewa na Ofisa habari wa Yanga Jerry Muro kuwa waliandikiwa barua ya kutaka kutoa ruhusa ya Kessy. Kessy amesajiliwa na Yanga akitokea Simba na amezuiwa kucheza kutokana na mkataba … Read More
  • ONYO KALI NA MUHIMU KWA YANGA KUELEKEA MECHI YAO LEOMwenyekiti wa zamani wa Simba Ismail Aden Rage amesema wachezaji wapya waliosajiliwa Yanga hawana leseni za kuichezea timu hiyo katika mchezo wa leo. Rage amesema Sheria ya Usajili ya michuano ya Kombe la shirikisho namba … Read More

0 comments:

Post a Comment