Tuesday, June 28, 2016

ONYO KALI NA MUHIMU KWA YANGA KUELEKEA MECHI YAO LEO

Mwenyekiti wa zamani wa Simba Ismail Aden Rage amesema wachezaji wapya waliosajiliwa Yanga hawana leseni za kuichezea timu hiyo katika mchezo wa leo.

Rage amesema Sheria ya Usajili ya michuano ya Kombe la shirikisho namba 4 na 5 inaonyesha kuwa wachezaji hao hawaruhusiwa kucheza kama hawajapewa leseni na kamati ya sheria na usajili ya shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Rage aliwataja wachezaji hao kuwa ni Hassan Kessy, Juma Mahadhi, Ben Kakolanya na Vicent Andrew.

"Kwa Mujibu wa sheria hizo za shirikisho la Soka Afrika (CAF) suala la usajili lina sehemu mbili. Wachezaji wanatakiwa kusajiliwa kabla ya januari 15 au kabla ya Agosti 10 ndipo waruhusiwe" alisema Rage.

Akifafanua zaidi suala hilo Rage amesema Yanga baada ya kufuzu michuano hiyo mapema,TFF kama ilikuwa inataka kuwasaidia Yanga, rais wake ambaye ni Jamal Malinzi alitakiwa kuitisha kikao cha dharula kufanya marekebisho ya kanuni za usajili kuisaidia timu hiyo kupata leseni za wachezaji hao. Kwa vile walishindwa kufanya hivyo sheria zinaeleza kuwa ili wachezaji hao waruhusiwe kucheza ni lazima wapitishwe na kamati hiyo ya TFF.

Aidha Rage aliongeza kuwa kamati hiyo haijakaa kwani utaratibu wao uliopo ni hadi kusubiri dirisha la usajili lifungwe kisha ikae na kupitia majina ambayo hayana pingamizi na ndipo iwaruhusu wachezaji hao kuitumikia klabu yao mpya.

Aliyewahi kuwa makamu wa rais  chini ya Uongozi wa Leodegar Tenga mwaka 2004 naye alisema "Ni lazima Yanga wawe makini kwenye hilo wasipoangalia inaweza kuwagharimu"

Hata hivyo habari zinasema kuwa TFF imeshampa leseni Kessy inayomwezesha kucheza katika mchezo wa leo dhidi ya Mazembe.

Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook Hapa

Related Posts:

  • HAYA NDO ALIYOAHIDIWA KOCHA PLUIJM YANGA Mkataba wa kocha mkuu wa Yanga Hans Pluijm ukiwa umebakiza siku chache kumalizika Yanga yafunguka juu ya kuendelea kubaki na kocha huyo. Klabu ya Yanga imeanza mazungumzo rasmi na kocha mkuu wa klabu hiyo Hans Van Pluijm… Read More
  • WENGER KUMWONGEZA MKATABA JACK WILSHERE Meneja Wa Arsenal Arsene Wenger Amepanga Kumwongezea Mkataba Mrefu Zaidi Wilshere. Arsene Wenger  ana mpango wa muda mrefu na Jack Wilshere hivyo kupanga kumwongezea mkataba utakaomuweka klabuni hapo kwa muda mrefu … Read More
  • SPURS NA ARSENAL KUWANIA SAINI YA MIDFIELD RAIA WA KENYA Tottenham Na Arsenal Wanasaka Saini Ya Midfieda Wa Southampton Victor Wanyama Wanyama alikuwa karibu kujiunga na Tottenham msimu uliopita lakini dili hilo lilifeli. Inasemekana Spurs bado wanania ya kumsajili Wanyama w… Read More
  • BRENDAN RODGERS KOCHA MPYA CELTIC Rodgers aliyetimuliwa na Liverpool mwezi October 2015 amechukua nafasi ya kocha Ronny Deila aliyeachia ngazi katika klabu ya Celtic ya nchini Scotland. Kocha huyo wa Zamani wa Liverpool na Swansea amesaini mkataba wa mie… Read More
  • HABARI KUBWA ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO MEI 19 Arsenal Imetenga Euro Milioni 65 Kumnasa Morata Klabu ya Arsenal imetenga kitita Cha Euro Milioni 65 kuhakikisha wanapata saini ya Morata anayetumikia klabu ya Juve kwa sasa. Sessegnon & Anichebe Kuondoka West Bro… Read More

0 comments:

Post a Comment