Friday, June 24, 2016

KIBARUA CHA LAURENT BLANC CHAOTA NYASI PSG

Klabu ya PSG imemtimua kocha wake Laurent Blanc, kwa mujibu wa jarida la la L'Equipe la nchini Ufaransa.

Taarifa za kutimuliwa kwa kocha huyo bado hazijawa rasmi kwani mpaka hivi sasa klabu ya PSG haijatoa tamko rasmi lakini kwa mujibu wa L'Equipe  tayari kocha huyo ashafungishwa virago.
Kwa mujibu wa gazeti hilo ni kwamba PSG walilazimika kumlipa Blanc Euro milioni 22 kwa kukatisha mkataba wake.

Kocha huyo ameshinda mataji 2 ya kombe la Ufaransa pamoja na makombe matatu ya ligi kuu katika misimu yake mitatu aliyoitumikia PSG, lakini rekodi zake mbaya katika michuano ya Klabu bingwa ulaya ndiyo iliyomfanya awashiwe taa za kijani klabuni hapo.

Wamiliki wa timu hiyo raia wa Quatar tamaa yao ni kuona PSG wakitwaa ubingwa wa Uefa Champions League kitu ambacho kocha Blanc ameshindwa kuwapa.

Habari za chini ya kapeti zinasema huenda kocha Unai Emery anaweza kurithi mikoba ya Blanc kwani kwa sasa hana klabu yoyote tangu abwage manyanga katika klabu ya Sevilla.

Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook Hapa

Related Posts:

  • TAYARI MOURINHO AMEMNASA ERIC BAILLY WA VILLARREAL Eric Bailly anakuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Jose Mourinho katika klabu ya Manchester United. Eric Bailly amekamilisha vipimo vya afya mapema leo na tayari beki huyo ameshasaini mkataba wa miaka 4 na klabu ya Man … Read More
  • MTIBWA HAITAMBUI USAJILI WA ANDREW VICENT YANGA Klabu ya Yanga hivi karibuni ilitangaza kumnasa mchezaji wa Mtibwa Sugar Andrew Vicent "Dante" lakini Msemaji wa Klabu ya Mtibwa, Thobias Kifaru amesema hana taarifa hizo. Klabu ya Mtibwa Sugar imesema haijapata taarifa j… Read More
  • HAWA NDIO WACHEZAJI 10 WANAOTAKIWA NA MOURINHO MAN U Mourinho ameshakabidhiwa mikoba katika klabu ya Man U na sasa atahitaji kufanya usajili kuimarisha kikosi hicho na kukirudisha katika level zake. Hawa ni wachezaji 10 ambao Mourinho anawataka  Manchester United; … Read More
  • USAJILI SIMBA NI TISHIOMwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu ya Simba, Zacharia Hans Pope ametamba kuwa wamejipanga kufanya usajili wa kisayansi zaidi lengo likiwa ni kupata kikosi imara kitakachowapa ubingwa msimu ujao. Kwa miaka mitatu mful… Read More
  • SIMBA YAMNASA WINGA MACHACHARI, ASAINI MIAKA 2 Klabu ya Simba Sports Club imefanikiwa kumsajili mchezaji wa Mwadui FC, Jamali Mnyate aliyesaini mkataba wa miaka 2 kwa uhamisho wa Tsh. Milioni 15. Kufuatia usajili huo Makamu Rais wa klabu hiyo, Geofrey Nyange Kaburu a… Read More

0 comments:

Post a Comment