Friday, June 24, 2016

CAF YAIFUTA ES SETIF KLABU BINGWA AFRIKA

Mabingwa mara mbili wa kombe la klabu bingwa Afrika, ES Setif wametolewa katika michuano hiyo kufuatia vurugu zilizofanywa na mashabiki wao.

Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF limeiondoa klabu ya ES Setif kwenye michuano ya klabu bingwa Afrika 2016.

Hatua hiyo inakuja kufuatia vurugu zilizosababishwa na mashabiki wa timu hiyo kwenye mchezo kati yao na klabu ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini.

Mashabiki hao walianzisha vurugu baada ya Tiyani Mabunda na Biliat Khama kufunga magoli mawili yaliyoifanya ya Mamelodi kuwa mbele kwa 2 - 0 katika mechi hiyo.

"(Maamuzi yamefanyika kufuatia vurugu zilizotokea katika mchezo namba 98 wa mwaka 2016 mechi ya klabu bingwa kati ya ES Setif (Algeria) dhidi ya Mamelodi Sundowns (Afrika Kusini), ambapo mwamuzi wa kati alilazimika kuahirisha mchezo huo kabla ya dakika tisini kumalizika" iliandikwa katika maelezo ya CAF.

Maofisa wa mchezo huo walisema waliona mashabiki wakirusha vitu uwanjani hapo kama vile, chupa, mawe na vitu vingine ambavyo vilisababisha majeraha kwa watazamaji wengine waliokuwepo uwanjani hapo kushuhudia mtanange huo pamoja na polisi waliokuwa wanalinda usalama wa mechi hiyo.

Bonyeza Hapa Ku-Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook



Related Posts:

  • CAF YAIFUTA ES SETIF KLABU BINGWA AFRIKAMabingwa mara mbili wa kombe la klabu bingwa Afrika, ES Setif wametolewa katika michuano hiyo kufuatia vurugu zilizofanywa na mashabiki wao. Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF limeiondoa klabu ya ES Setif kweny… Read More
  • KIKOSI CHA YANGA LEO DHIDI YA TP MAZEMBEKIKOSI CHA YANGA LEO. 1. Deogratius Bonaveture Munishi 'Dida' 2.Juma Abdul Mnyamani. 3. Mbuyu Twite Junior. 4. Kelvin Patrick Yondani "Cotton" 5. Vicent Bossou. 6. Thaban Michael Kamusoko. 7. Juma Mahadhi. 8. Haruna Fadhil… Read More
  • YANGA KULIPA ZAIDI YA MILION 500 CAFKlabu ya Yanga imetakiwa kulipa fidia ya Tsh. milioni 530 kama fidia ya gharama za mchezo wao dhidi ya TP Mazembe baada ya kuruhusu mashabiki kuingia bure uwanjani. CAF na TFF imefikia hatua hiyo baada ya Yanga kufuta kiin… Read More
  • CAF YAIBEBA YANGA KUELEKEA MECHI NA MAZEMBEShirikisho la Mpira wa miguu barani Afrika CAF, limewaidhinisha wachezaji watatu wa Yanga ambao walikuwa wanatumikia adhabu ya kadi kucheza, kucheza katika mchezo wao na TP Mazembe. Wachezaji wa Yanga, Oscar Joshua, Nadir … Read More
  • HII NDO HALI ILIYOPO UWANJA WA TAIFA WATU WAMEFURIKA Kuelekea Mchezo kati ya Yanga na TP Mazembe Leo Jioni Hivi Ndivyo Mashabiki Walivyofurika Uwanja Wa Taifa Mapema Leo Kusubiri Mchezo Huo. KILA LA KHERI YOUNG AFRICA Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook Hapa … Read More

0 comments:

Post a Comment