Sunday, May 15, 2016

VITA YA KUWANIA NAFASI YA PILI VPL KUENDELEA TENA LEO


LIGI kuu Tanzania bara inatarajia kuendelea tena leo katika viwanja viwili. Mjini Morogoro wakata miwa wa Mtibwa watawakaribisha vijana wa Msimbazi Simba SC wakati huko Tanga Azam FC itachuana na African Sports.
Simba wanashika nafasi ya 3 katika msimamo wa ligi wakiwa wamejikusanyia pointi 59 katika michezo 28 waliyocheza, wakati Azam FC wao wapo katika nafasi ya 2 kwa jumla ya pointi 63 walizozipata katika michezo 28 waliyocheza.

Timu hizi zitashuka viwanjani leo zote zikiwa na dhamira ya kupata ushindi ili kuweza kuzipata milioni 40 anazopewa mshindi wa pili wa ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom Premier League, endapo Azam FC watashinda mchezo wa leo basi moja kwa moja watakuwa washindi wa pili kwa kuibwaga Simba SC kwani watakuwa wamefikisha pointi 66 huku wakibakiwa na mchezo mmoja, wakati huo Simba wao wakishinda mechi ya leo watafikisha pointi 62 na kubakiwa na mchezo mmoja ambao hata wakishinda watafikisha pointi 65 wakiachwa kwa pointi 1 na Azam FC.

Hali hii ndo inazifanya mechi za leo kuwa ni za kuvutia licha ya kuwa bingwa tayari alishapatikana na kukabidhiwa kombe lake. Azam FC watakuwa wanapambana kupata ushindi katika mchezo wake leo, Simba nao watapigana vikali kuhakikisha wanashinda huku wakiwaombea wapinzani wao Azam FC kupoteza katika mchezo wao dhidi ya African Sports.


Related Posts:

  • Hapatoshi Leo Tena Taifa Patashika za ligi kuu ya kandanda tanzania bara zinaendelea tena leo kwa mchezo mmoja tu kupigwa katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam ukiwakutanisha wenyeji Simba SC dhidi ya Toto Africans ‘wana kishamapanda’kutok… Read More
  • Abdi Banda Alia Na Viongozi Wa Simba Mchezaji wa Simba Abdi Banda anasema hajui mustakabali wake katika Klabu hiyo kufuatia tamko la adhabu aliyopewa kutokana  na kupishana kauli na kocha wake Jackson Mayanja katika mechi dhidi ya Coastal Union. Ana… Read More
  • Tambwe Amechuja Awekwe Benchi Mashabiki wa Klabu ya Dar Young Africans wameonyesha kutokufurahishwa na kiwango kinachoonyeshwa na mshambuliaji wao Amis Tambwe siku za hivi karibuni. Tambwe ambe ana magoli 18 katika orodha ya wafungaji bora msimu huu an… Read More
  • Hiki Ndio Kikosi Cha Yanga Leo Dhidi Ya Mtibwa Sugar LIGI KUU || TZ - BARA || 2015~2016. YANGA SC Vs MTIBWA SUGAR FC. UWANJA - Uwanja wa Taifa. Muda - saa 10 : 00Alasiri. >>>>>>KIKOSI CHA YANGA LEO<<<<<<<< 1. Deogratias Bonave… Read More
  • Mnyama Achinjwa Taifa Timu ya soka ya Simba imezidi kupoteza matumaini ya kunyakua ubingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara baada ya kukubali kichapo cha Goli 1 - 0 toka kwa Toto Africans ya Mwanza.Katika mchezo huo ambao wadau wengi wa soka waliip… Read More

0 comments:

Post a Comment