Patashika za ligi kuu ya kandanda tanzania bara zinaendelea tena leo kwa mchezo mmoja tu kupigwa katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam ukiwakutanisha wenyeji Simba SC dhidi ya Toto Africans ‘wana kishamapanda’kutoka jijini Mwanza.
Mchezo huo unatarajiwa kuwa mgumu kwa pande zote,ambapo Simba inataka kurejea kwenye kiti chake cha enzi kileleni kwa kufikisha pointi 60 huku Toto Africans wakitaka kujinyanyua kuukwepa mstari wa kuporomoka daraja kutoka katika nafasi ya 11 iliyopo sasa.
Simba kwa sasa inashikilia nafasi ya pili ikiwa na pointi 57 nyuma ya Yanga wenye pointi 59 huku Azam FC wakishikilia nafasi ya tatu kwa kuwa na pointi 55.
Kwa mujibu wa kocha wa Saimba,Jackson Mayanja,amesema vijana wake wapo tayari kukusanya pointi zote zilizobakia ili kumaliza wa kwanza na hatimae kushiriki michuano ya klabu bingwa barani afrika msimu ujao.
Related Posts:
BREAKING NEWS: AZAM FC YAPOKWA POINTI 3 NA MAGOLI 3
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Alfred Lucas, amesema katika mechi namba 156 iliyozikutanisha Mbeya City dhidi ya Azam kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya, Azam ilimchezesha Nyoni kinyume na … Read More
YANGA BINGWA TENA 2015/16
MCHEZO Kati ya Simba SC na Mwadui FC umemalizika kwa Mwadui kuibuka na ushindi wa goli 1 - 0. Simba walikuwa wanahitaji kushinda katika mechi hii ili kuisubirisha Yanga kutangaza ubingwa mapema, lakini hilo limeshindikan… Read More
AZAM FC KUTUPA KARATA YAKE TENA DHIDI YA KAGERA SUGAR
KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, inatarajia kuondoka kuelekea mkoani Mwanza kwa ajili ya kupambana na Kagera Sugar kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) utakaofanyika Uwanja wa Kambara… Read More
SIMBA YAIFUATA MAJIMAJI SONGEA
Kikosi cha Simba kimesafiri alfajiri ya leo kuelekea Songea tayari kwa mchezo wake dhidi ya Majimaji FC. Simba itaingia katika mchezo huu ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo wake wa awali dhidi ya Mwadui FC, hivyo kuh… Read More
MECHI 2 KALI ZA KUZITAZAMA LEO LIGI KUU TANZANIA BARA
SIMBA SC VS MWADUI FC
Simba leo wanawakaribisha Mwadui FC katika mchezo wa 27 wa
Ligi kuu Tanzania Bara, Simba wanaingia katika mechi hii wakiwa na rekodi mbaya
katika mechi za hivi karibuni, kwanii hutakiwi kukosa ku… Read More
0 comments:
Post a Comment