Monday, May 16, 2016

VICENT BOSSOU AITWA TIMU YA TAIFA YA TOGO


Kocha mpya wa Togo Mfaransa Claude LeRoy amemuita Vicent Bossou katika kikosi cha timu yake ya Taifa .Bossou ameitwa kutokana na kiwango kizuri alichokionyesha akiwa na klabu ya Yanga.

Tayari barua ya mualiko wa kujiunga na timu ya taifa lake imeshafika Yanga katika ofisi ya katibu wao Baraka Deusdedit kwa beki huyo kujiunga na timu hiyo itakayoingia kambini wiki chache zijazo kuumana na Liberia.

“Kweli nimeitwa kujiunga na timu ya taifa, Yanga wameshapokea barua hiyo ya mualiko na kunijulisha, kwangu ni taarifa nzuri kwa kuwa nakwenda kulisaidia taifa langu baada ya kuisaidia klabu yangu kutwaa ubingwa sasa najiunga na taifa langu,” amesema Bossou.

Mara ya mwisho kwa Bossou kuitwa Togo ni wakati kikosi hicho kikicheza na Uganda wakati huo ikifundishwa na kocha Mbelgiji Torm Saintfiet ambaye hata hivyo hakumchezesha hata mara moja.

Related Posts:

  • Azam Fc Kuifuata Esperance De Tunis KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, inatarajia kuondoka leo kuelekea jijini Tunis kwa ajili ya kukabiliana na Esperance ya huko kwenye mchezo wa marudiano wa raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho Afrika utaka… Read More
  • LIVE KUTOKA TAIFA - FUATILIA LIVE MCHEZO KATI YA SIMBA NA TOTO AFRICANS HALF TIME MATOKEO: SIMBA 0 - 1 TOTO AFRICANS Mfungaji: Wazir Junior  ======== KIPINDI CHAPILI KIMEANZA Dakika ya 47: beki wa Simba, Hassan Kessy anapewa kadi nyekundu kwa kumchezea faulo, Edward Chris… Read More
  • TFF Yatuma Salamu Za Rambirambi MZFA Shirkisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetuma salamu za rambirambi kwa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Mwanza (MZFA), kufuatia kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti mstaafu wa MZFA na makamu mwenyekiti wa FAT Silvanus Maka… Read More
  • Hapatoshi Leo Tena Taifa Patashika za ligi kuu ya kandanda tanzania bara zinaendelea tena leo kwa mchezo mmoja tu kupigwa katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam ukiwakutanisha wenyeji Simba SC dhidi ya Toto Africans ‘wana kishamapanda’kutok… Read More
  • Tanzania Yazidi Kupata Umaarufu Duniani Bondia Ibrahim Class Bondia mtanzania Ibrahim Class ‘King Class Mawe’ameendelea kutamba katika mapigano yake nje ya nchi baada ya usiku wa kuamkia jana kufanikiwa kumtwanga Mjerumani huko Panama City Amerika Kusini. … Read More

0 comments:

Post a Comment