Saturday, May 28, 2016

MANENO YA HANS POPE KWA DONALD NGOMA

Hans Pope bosi anayeshughulikia maswala ya Usajili kunako klabu ya Simba ameweka bayana kuvutiwa kwake na Mshambuliaji wa Yanga Donald Ngoma.




Hans Pope amesema licha ya Amiss Tambwe kuibuka Mfungaji bora katika msimu wa ligi uliomalizika hivi karibuni kwake yeye anawakubali wachezaji wawili tu. Akizungumza na Gazeti la Mwanaspoti Hans alisema mshambuliaji wa Yanga Donald Ngoma na Kiungo wa Simba Justice Majabvi ndio wachezaji pekee anaowakubali kutokana na uwezo wao mkubwa wanapokuwa uwanjani, Huku akisisitiza kwamba Ngoma ndiye Mkali zaidi ya wote.

"Simba bila wasiwasi nitamtaja Majabvi, amekuwa na msaada mkubwa sana katika timu yetu lakini nje ya Simba kwa Azam namuona Kipre Tchetche yuko vizuri." alisema Hans Pope.

"Lakini Ukiangalia kwa Ujumla yule Mshambuliaji wa Yanga, Ngoma amekuwa kivutio kikubwa, ni mchezaji anayeweza akatengeneza goli la kwake si aina ya washambuliaji ambaye anaweza kutegemea mipira ya kulishwa" aliongeza Hans Pope.

Simba imemaliza ligi katika nafasi ya tatu na Hans Pope kama bosi wa kamati ya Usajili klabuni hapo ameshawahi kupitia wakati mgumu katika ligi kuu Msimu huu pale mashabiki walipokamzingira wakionyeshwa kukerwa kwao na muenendo wa timu yao pale Simba ilipofungwa na Toto Africans katika mchezo wa ligi msimu huu. Kutokana na hali hiyo Uongozi wa Simba kwa sasa unahaha kutafuta wachezaji wazuri watakaoimarisha sawasawa kikosi chao tayari kwa kuleta ushindani mkubwa katika msimu ujao wa ligi.

Related Posts:

  • Azam Fc Kuifuata Esperance De Tunis KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, inatarajia kuondoka leo kuelekea jijini Tunis kwa ajili ya kukabiliana na Esperance ya huko kwenye mchezo wa marudiano wa raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho Afrika utaka… Read More
  • Hiki Ndio Kikosi Cha Yanga Leo Dhidi Ya Mtibwa Sugar LIGI KUU || TZ - BARA || 2015~2016. YANGA SC Vs MTIBWA SUGAR FC. UWANJA - Uwanja wa Taifa. Muda - saa 10 : 00Alasiri. >>>>>>KIKOSI CHA YANGA LEO<<<<<<<< 1. Deogratias Bonave… Read More
  • TFF Yatuma Salamu Za Rambirambi MZFA Shirkisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetuma salamu za rambirambi kwa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Mwanza (MZFA), kufuatia kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti mstaafu wa MZFA na makamu mwenyekiti wa FAT Silvanus Maka… Read More
  • Misri Waihofia Stars AFCON Timu ya taifa ya Misri katika kile kinachoonekana kupania kuiondoa Taifa Stars katika michuano ya kufuzu mashindano ya Afcon 2017, wapo nchini kuifuatilia Stars kila hatua. Taarifa zinasema Meneja wa Timu hiyo yupo nchi… Read More
  • Tanzania Yazidi Kupata Umaarufu Duniani Bondia Ibrahim Class Bondia mtanzania Ibrahim Class ‘King Class Mawe’ameendelea kutamba katika mapigano yake nje ya nchi baada ya usiku wa kuamkia jana kufanikiwa kumtwanga Mjerumani huko Panama City Amerika Kusini. … Read More

0 comments:

Post a Comment