Saturday, April 16, 2016

Misri Waihofia Stars AFCON


Timu ya taifa ya Misri katika kile kinachoonekana kupania kuiondoa Taifa Stars katika michuano ya kufuzu mashindano ya Afcon 2017, wapo nchini kuifuatilia Stars kila hatua.

Taarifa zinasema Meneja wa Timu hiyo yupo nchini akiilia rada Stars katika kuhakikisha wanaifunga Stars katika mechi yao ya marudiano.

“Meneja wa Misri yupo nchini tangu Jumatano iliyopita na TFF (Shirikisho la Soka Tanzania) wanazo taarifa za ujio wake, huyu amekuja kuandaa mazingira ya timu itakapofikia na mambo mengine.

“Inavyoonekana wamepania kufuzu fainali hizi na ndiyo maana wameonekana kuanza maandalizi ya mchezo huo ikiwa ni miezi miwili kabla,” alisema mtoa taarifa huyo.

0 comments:

Post a Comment