Thursday, March 23, 2017

FERGUSON: Ronaldo na Messi, wakizeeka Soka la hispania litadorora


Kocha wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson anaamini soka la Hispania litakoma kutawala ulaya katika ngazi ya vilabu.

Katika kipindi cha miaka nane iliyopita vilabu vya Hispania vimetwaa kombe la ligi ya mabingwa ulaya ‘UEFA Champions league’ mara 5, achilia mbali kombe la EUROPA ambapo Sevilla imelichukua mara tatu mfululizo katika miaka hiyo.

Sir Alex Ferguson amesema kuwa vilabu vya nchi Fulani kuwa na mafanikio huwa ni kipindi cha mpito na akatoa mifano ya wazi.

Mfano miaka ya1970  Ajax na Bayern Munich ndio walikuwa vinara wa kubeba kombe hilo, miaka ya 1980 ikawa zamu ya Liverpool , miaka 1990 Italy na AC Milan walitwaa zaidi kombe hilo wakati.
Pia hakusita kuitaja Manchester United katika kipindi cha miaka 4 ndani ya miaka sita iliyopita Manchester ilicheza fainali tatu.

“Naamini sasa ni zamu ya vilabu vya Hispania kutawala, ni timu bora na ndio maana zinatawala. Lakini mambo yatabadilika kama yanavyobadilika, unajua Ronaldo na Messi watazeeka, je nani m’badala wao? Hivyo nadhani mzunguko utaendelea. ”

Vilabu vitatu vya Hispania vimefuzu katika hatua ya Robo fainali ya ligi ya mabingwa, vilabu hivyo ni bingwa mtetezi wa kombe hilo Real Madrid, Barcelona na Atletico Madrid.
Real Madrid itakutana na Bayern Munich
Barcelona watakutana na Juventus

Atletico Madrid watakutana na Leicester City.

Related Posts:

  • Manchester City 2 - 1 Swansea City, Gabriel Jesus aipeleka city nafasi ya tatu EPL Etihad Stadium Manchester City imeitandika  Swansea City goli 2 -1 katika mchezo mkali na wakusisimua. Kitu kizuri kwa Manchester city ni ujio wa mshambuliji Gabriel Jesus ambae ameongeza changamoto kwa Ser… Read More
  • Samatta kazini leo Ubeligiji KRC Genk leo inashuka katika dimba lake la nyumbani la Luminus Arena kumenyana na timu inayoburuza mkia katika Belgium - Pro League timu iitwayo Royal Excel Mouscron. Mchezo utakaopigwa saa 22:00 majira ya Afrka Masharik… Read More
  • Mkongwe Chelsea Amchana John Terry Marcel Desailly beki wa zamani wa Chelsea amemwambia John Terry kwamba muda wake umekwisha Chelsea. Desailly anaaamini kuwa muda wa Terry kuondoka Chelsea umewadia na ni kutokana na kukosa nafasi kwenye kikosi cha kwanza … Read More
  • Leicester yakubali yaishe kwa Man U, yatota 3 - 0 King Power Stadium Ikicheza kwa kujiamini muda wote Manchester United imeitandika Leicester-city bila huruma goli 3 – 0 katika dimba la King Power huko Leicester. Ilibidi united wasubiri mpka dakika 41 ndio waanze ku… Read More
  • chelsea vs Arsenal, Stamford Bridge Ikiwa imetoka  kusuluhu na Liverpool, Chelsea itataka kujihakikishia nafasi ya kutwaa kombe pale tu itakapoweza kupata Matokeo chanya mbele ya Arsenal Arsenal inaingia uwanjani Stamford Bridge kwa lengo moja … Read More

0 comments:

Post a Comment