Kocha wa zamani wa
Manchester United Sir Alex Ferguson anaamini soka la Hispania litakoma kutawala
ulaya katika ngazi ya vilabu.
Katika kipindi cha
miaka nane iliyopita vilabu vya Hispania vimetwaa kombe la ligi ya mabingwa
ulaya ‘UEFA Champions league’ mara 5, achilia mbali kombe la EUROPA ambapo
Sevilla imelichukua mara tatu mfululizo katika miaka hiyo.
Sir Alex Ferguson
amesema kuwa vilabu vya nchi Fulani kuwa na mafanikio huwa ni kipindi cha mpito na
akatoa mifano ya wazi.
Mfano miaka ya1970 Ajax na Bayern Munich ndio walikuwa vinara wa
kubeba kombe hilo, miaka ya 1980 ikawa zamu ya Liverpool , miaka 1990 Italy na
AC Milan walitwaa zaidi kombe hilo wakati.
Pia hakusita kuitaja
Manchester United katika kipindi cha miaka 4 ndani ya miaka sita iliyopita Manchester
ilicheza fainali tatu.
“Naamini sasa ni zamu
ya vilabu vya Hispania kutawala, ni timu bora na ndio maana zinatawala. Lakini mambo
yatabadilika kama yanavyobadilika, unajua Ronaldo na Messi watazeeka, je nani m’badala
wao? Hivyo nadhani mzunguko utaendelea. ”
Vilabu vitatu vya
Hispania vimefuzu katika hatua ya Robo fainali ya ligi ya mabingwa, vilabu
hivyo ni bingwa mtetezi wa kombe hilo Real Madrid, Barcelona na Atletico Madrid.
Real Madrid itakutana
na Bayern Munich
Barcelona watakutana
na Juventus
Atletico Madrid
watakutana na Leicester City.
0 comments:
Post a Comment