Saturday, June 18, 2016

KIPAUMBELE NAMBA 1 CHA SIMBA KATIKA USAJILI HIKI

Simba ipo katika harakati za kuimarisha kikosi chao kwa kuhakikisha hawafanyi makosa katika usajili kipindi hiki ambacho dirisha la usajili limefunguliwa.

Uongozi wa Simba umesema kipaumbele chao cha kwanza katika kipindi hiki cha usajili ni kocha, wanataka wampate kocha mwenye rekodi nzuri ambaye pia atawasaidia katika kuwasajili wachezaji wazuri, Mwenyekiti wa klabu hiyo Evans Aveva amebainisha hilo kwa kusema lengo ni kushirikiana na kocha huyo katika kufanya usajili ambao utakuwa ni wa uhakika.

"tunaona suala la kocha liwe namba moja, wachezaji tayari tumeanza kusajili vizuri lakini itapendeza kama tutakuwa na ushirikiano wa karibu na mkuu wa benchi la ufundi maana wao ndiyo wataalamu zaidi yetu." alisema Aveva.

Bosi wa kamati ya usajili Zacharia Hans Poppe alisafiri kwenda nchini Zimbabwe kujaribu kuzungumza na kocha anayeifundisha timu ya taifa ya Zimbabwe, Kalisto Pasuwa lakini juhudi hizo ziligonga mwamba na kumkosa kocha na kuamaua kuongeza kasi za kusaka kocha mwingine.

Bonyeza hapa ku-Like Page ya Soka24 Facebook

Related Posts:

  • MIPANGO YA JULIO KATIKA USAJILIKocha wa Mwadui FC, Jamhuri Kiwelu "Julio" amesema yeye hana mpango wa kusajili wachezaji wa kigeni katika kikosi chake. Julio amesema lengo lake ni kutoa fursa kwa wachezaji wa ndani waweze kuonyesha uwezo wao ili waje ku… Read More
  • SIMBA WAZIDI KUWEKA NGUMU KWA YANGA KUHUSU KESSYKlabu ya Simba imesema kama si Yanga kuwapatia fedha hawataandika barua itakayomuidhinisha Hassan Ramadhan Kessy kucheza michuano ya Kombe la shirikisho CAF CC Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa kamati ya Usajili wa Simba, Za… Read More
  • SHOMARI KAPOMBE KURUDI MSIMBAZIKlabu ya Simba imesema inapambana kuhakikisha wanamrudisha kikosini beki wao Shomari Kapombe anayeitumikia klabu ya Azam FC kwa sasa. Kapombe ambaye hivi karibuni ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa msimu uliopita ligi kuu Vo… Read More
  • KIMESHAELEWEKA YANGA WAPYA WOTE RUKSA ISIPOKUWA HUYUWachezaji wote wapya wa Yanga wamethibitishwa kuwa huru kuanza kuitumikia klabu hiyo isipokuwa Hassan Ramadhan Kessy. Yanga imewasajili wachezaji watano hadi sasa ambao ni Andrew Vicent, Juma Mahadhi, Ben Kakolanya, Hassan… Read More
  • TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO JUMATANO JUNI 22,2016Tetesi Za Usajili Barani Ulaya  Bale Kupewa Mkataba Mrefu Madrid Mchezaji wa kimataifa wa Wales, Gareth Bale anatarajiwa kupewa mkataba mpya utakaomuweka Santiago Bernabeu Kwa zaidi ya miaka 6. Barcelona Yamuwinda Ga… Read More

0 comments:

Post a Comment