BEKI kisiki wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Shomari Kapombe, ameondoka nchini leo saa 9.35 Alasiri akielekea Afrika Kusini kwa ajili ya kutibiwa kifua ambacho kinamsumbua.
Kapombe aliyekosa mechi mbili zilizopita za Azam FC dhidi ya Toto Africans na Ndanda, alianza kuumwa na kifua wakati kikosi hicho kikijiandaa kuvaana na Toto jijini Mwanza kabla ya kukimbizwa hospitalini.
Awali beki huyo alikuwa akisumbuliwa na homa kali ya mafua ambayo pia iliwaathiri baadhi ya wachezaji wa Azam FC waliotoka nchini Chad kwenye kambi ya Taifa Stars akiwemo nahodha John Bocco ‘Adebayor’ na hiyo ni kutokana na hali mbaya ya hewa iliyoko jijini N'Djamena.
Kapombe ameelekea nchini humo sambamba na Daktari wa timu, Dr. Juma Mwimbe, ambapo mara baada ya kuwasili kesho wataelekea kwenye Hospitali ya Morningside Mediclinic iliyopo jijini Johannesburg kwa ajili ya beki huyo kuanza kufanyiwa vipimo ili kubainika tatizo.
“Kapombe anasikia maumivu ya kifua na mara kwa mara amekuwa akilalamika mbavu zinamuuma, tunashukuru Mungu kwa sasa hali yake inaendelea vizuri tofauti na awali, ila tunachoenda kufanya huko ni kuangaliwa zaidi ni kinamsumbua kwa kuchukuliwa vipimo na baadaye ndio itajulikana kitaalamu ni kinamsumbua,” alisema Mwimbe wakati akizungumza na mtandao wa klabu www.azamfc.co.tz dakika chache kabla hawajaelekea huko na ndege ya Shirika la Afrika Kusini.
Beki huyo wa zamani wa Simba na AS Cannes ya Ufaransa, amekuwa mmoja wa wachezaji tegemeo wa Azam FC msimu huu kwenye mechi mbalimbali alizocheza, akiwa mpaka sasa amefunga jumla ya mabao 11 kwenye michuano yote, nane katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL).
Mabao mengine mawili amefunga kwenye Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) huku moja akifunga katika Kombe la Shirikisho Afrika (CC) dhidi ya Bidvest Wits walipoichapa 3-0 jijini Johannesburg kabla ya kufuzu raundi ya pili ya michuano hiyo kwa jumla ya mabao 7-3 na sasa itakutana na Esperance de Tunis Jumapili ijayo (Aprili 10) na mchezo wa marudiano jijini Tunis Aprili 20.
Chanzo: Azam fc official site.
Thursday, April 7, 2016
Kapombe Akimbizwa Sauzi Kwa Matibabu
Related Posts:
YA LWANDAMINA NA KIBARUA CHAKE YANGA Kocha Mkuu wa Yanga George Lwandamina amesema kazi ya ukocha inahitaji uwepo wa kikosi chenye vipaji tofauti na uwezo husika. Lwandamina aliyejiunga na Yanga akitokea Zesco ya nchini Zambia, tangu kutua kwake mashabiki na wa… Read More
YANGA YAWALISHA KWATA MAAFANDE WA JKT RUVU Mchezo wa kwanza wa raundi ya pili ligi kuu Tanzania bara uliowakutanisha Yanga na JKR umemalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi mnono wa magoli matatu kwa bila. Magoli ya Yanga yamefungwa na Michael Aidan 38' (Goli la ku… Read More
KIKOSI CHA YANGA DHIDI YA NDANDA FC LEO LIGI KUU TANZANIA BARA MZUNGUKO WA PILI Yanga v Ndanda FC Muda: Saa 10:00 Jioni (Jumatano, Disemba 28, 2016)Uwanja: Uhuru Stadium Kikosi Cha Yanga 1.Deogratius Munishi 2.Juma Abdul 3.Mwinyi Haji 4.Vicent Bo… Read More
BREAKING NEWS: AZAM FC YASIMAMISHA BENCHI LAKE LOTE LA UFUNDI Klabu ya Azam FC imesimamisha uongozi wa benchi lake lote la Ufundi akiwemo kocha Mkuu Zeben Hernandez. Kocha wa Muda atatangazwa hivi punde. Habari zaidi itakujia hivi punde.............................. … Read More
Mechi Za Leo Jumamosi Januari 28 VPL 2016/17 Ligi kuu Tanzania Bara (VPL) inataraji kuendelea tena leo kwa michezo mitatu itakayotimua vumbi katika mikoa ya Dar, Mbeya na Mtwara.Ratiba Kamili ni kama inavyoonekana hapa chini; Dar Es Salaam Simba V Azam FC Mbeya Ta… Read More
0 comments:
Post a Comment