Thursday, May 5, 2016

FARID MUSSA AFUZU MAJARIBIO HUKO NCHINI HISPANIA


Mchezaji wa Azam FC Farid Mussa aliye nchini Hispania alikokwenda kwa lengo la kufanya majaribio katika klabu ya Deportivo Tenerife inayoshiriki Ligi Daraja la kwanza, amefanikiwa kufuzu majaribio hayo na sasa Uongozi wa klabu hiyo utakaa mezani na Azam FC ili kukamilisha usajili wake.

“Tunatarajia kuanza mazungumzo nao juu ya suala la Farid, ingawa wazo lao la awali ni kumchukua kwa mkopo wa miaka miwili. Sasa tunasubiri ofa yao rasmi, kisha Bodi ya Ukurugenzi itajadili na kutoa maamuzi,”amesema Yusuf Bakhresa Mkurugenzi wa Azam FC.

Faridi ambaye wakati anaondoka nchini alitegemewa kwenda kufanya majaribio katika klabu za Las Palmas na Athletic Club zinazoshiriki ligi kuu Nchini humo maarufu kama La Liga, lakini wakala wake alishauri afanye majaribio katika timu ambayo inashiriki ligi daraja la kwanza lengo likiwa ni kumwezesha kupata nafasi ya kucheza mara kwa mara ili kuimarisha kipaji chake na kuonekana na klabu kubwa za ligi kuu Nchini humo na Ligi zingine kubwa duniani.

KILA LA KHERI FARID MUSSA

Related Posts:

  • FAINALI COPA AMERICA 2016 NI CHILE VS ARGENTINA Timu ya taifa ya Chile imefanikiwa kuibuka na ushindi wa magoli 2 - 0 dhidi ya Colombia katika mchezo wa nusu fainali Copa America 2016 na kufanikiwa kutinga fainali ya michuano hiyo na sasa watakutana na Argentina kwa m… Read More
  • ARGENTINA YATINGA FAINALI MESSI AWEKA REKODI COPA AMERICA Lionel Messi ameweka Rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote katika kikosi cha Argentina baada ya kufunga goli katika mechi ya robo fainali michuanoo ya Copa America dhidi ya Marekani, Mechi iliyomalizika alfajiri ya Le… Read More
  • YANGA TAYARI KWA KUIVAA MO BEJAIA Timu Ya Yanga imeshawasili nchini Algeria tayari kwa kuwavaa MO Bejaia katika mchezo wa kwanza hatua ya makundi kombe la shirikisho barani Afrika CAF CC, utakaofanyika siku ya kesho Jumapili juni 19, 2016 … Read More
  • IBRAHIMOVIC ATANGAZA KUSTAAFU SOKAZlatan Ibrahimovic 34, amesema atastaafu kuitumikia timu yake ya taifa baada ya kumalizika kwa michuano ya Euro 2016' Ibrahimovic amesema mechi yake ya mwisho ni kati ya Sweden na Ubelgiji itakayochezwa Jumatano. Sweden it… Read More
  • CAF YAIFUTA ES SETIF KLABU BINGWA AFRIKAMabingwa mara mbili wa kombe la klabu bingwa Afrika, ES Setif wametolewa katika michuano hiyo kufuatia vurugu zilizofanywa na mashabiki wao. Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF limeiondoa klabu ya ES Setif kweny… Read More

0 comments:

Post a Comment