Sunday, May 15, 2016

ACACIA KUSITISHA UDHAMINI NA STAND UNITED


KAMPUNI ya ACACIA inayoidhamini timu ya Stand United ya mkoani Shinyanga imesema itaondoa udhamini wake na klabu ya Stand kama Stand itaendeshwa kama kampuni. Taarifa hizo zimekuja mara baada ya Stand kutangaza kuwa kwa sasa itaendeshwa kama kampuni tofauti na ilivyokuwa awali.Baada ya taarifa hizo kuifikia kampuni hiyo ya ACACIA, uongozi wa kampuni umeiandikia uongozi wa klabu ya Stand United barua inayowataarifu Stand juu ya ACACIA kutaka kusitisha udhamini wao na klabu hiyo kama Stand itaendeshwa kama kampuni.

Mwenyekiti wa Stand United Amani Vicent amethibitisha kupokea barua hiyo kutoka katika kampuni ya ACACIA huku akikiri kuwa ni kweli kwamba Stand kwa sasa itaendeshwa kama kampuni huku akidai kuwa uongozi wa Stand utakaa na Mabosi wa ACACIA ili kuweka mambo sawa lengo likiwa ni kuwaomba wasisitishe udhamini wao licha ya ukweli kuwa Stand ni kampuni na itabaki kuwa hivyo.

Itakumbukwa kuwa kampuni ya ACACIA iliingia udhamini na klabu ya Stand United mara baada ya kumalizika kwa msimu wa ligi wa mwaka 2014/15, udhamini wenye thamani ya  shilingi bilioni 2.4 kwa muda wa miaka miwili.

Related Posts:

  • OMOG ASHUSHA PRESHA ZA WANAMSIMBAZI Kocha wa klabu ya Simba, Mcameroon, Joseph Omog amewataka mashabiki wa klabu hiyo kuwa watulivu kufuatia sare ya bila kufungana waliyoipata dhidi ya JKT Ruvu. Omog amesema hayo ni matokeo ya kawaida ya kimchezo hivyo mash… Read More
  • AZAM VS SIMBA KUPIGWA DIMBA LA UHURU Mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) kati ya Azam FC na Simba ya Dar es Salaam, utafanyika Jumamosi Septemba 17, 2016 kama ilivyopangwa awali. Ila mchezo huo utafanyika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam badala y… Read More
  • YANGA WAPATA ENEO LA UWANJA Hatimae yanga yapata kibali cha kujenga uwanja wao katika manispaa ya kigamboni baada ya kusubiri michakato kwa muda mrefu sana. hayo yamethibitishwa na mtu wa ndani wa kilabu ya yanga hapo jana. eneo hilo lina hekari zaid… Read More
  • BOCCO AITISHIA NYAU SIMBA ZIKIWA zimesalia siku tatu kabla ya kupambana na Simba, Nahodha wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, John Bocco ‘Adebayor’, amesema kuwa wanamorali kubwa ya kuibuka na ushindi katika mchezo huo utakaofanyika … Read More
  • SIMBA YABADILI GIA ANGANI Sare ya bila kufunguna waliyoipata Simba dhidi ya JKT Ruvu imemfanya kocha wa klabu hiyo, Joseph Omog kubadili mfumo wa uchezaji na kusisitiza umakini kwa wachezaji katika mechi zijazo. Katika mchezo huo dhidi ya JKT Ruvu… Read More

0 comments:

Post a Comment