Friday, June 2, 2017

Simba Wapata Mbadala Wa Juuko Murshid

Munezero Fiston ni Mnyarwanda ambaye yupo katika mipango ya Simba baada ya kocha Joseph Omog kupendekeza atafutiwe mchezaji mwingine.


Munezero, anayekipiga katika klabu ya Rayon Sport anatarajiwa kutua Dar Es Salaam Jumamosi hii kwa lengo la kufanya mazungumzo na wekundu hao wa Msimbazi.

Hatua hii inakuja baada ya taarifa za kuomba kuondoka kwa beki Juuko Murshid pamoja na hali ya majeraha inayomsumbua Method mwanjali hivyo kuonekana kuna kila sababu ya kupata mbadala wa nyota hao.


“Munezero atawasili rasmi Jumamosi hii. Tunaweza kumtumia kwenye michuano ya Super Cup, mashabiki wetu watapata nafasi ya kumuona hapo,” kilisema chanzo kimoja cha habari.

Pamoja na beki huyo, Simba ina mpango wa kusajili wachezaji wengine watatu, ambao ni kiungo, mshambuliaji na beki mwingine kujenga ukuta imara kwenye kikosi hicho.

Related Posts:

  • TAARIFA ZA USAJILI: Barani Ulaya Mancini Atua Zenit Kocha wa zamani wa klabu ya Manchester City, Roberto Mancini amekabidhiwa rasmi mikoba ya kuinoa klabu ya Zenit ya nchini Urusi. Mancini anachukua nafasi ya Mircea Lucescu. Rasmi: Huntelaar arudi Ajax … Read More
  • VIKOSI SIMBA, YANGA BAADA YA USAJILI DIRISHA DOGO Dirisha Dogo la Usajili limefungwa rasmi jana Alhamisi Disemba 15 majira ya Saa 6:00 usiku. Soka24 imefanikiwa kuvinasa vikosi vya miamba ya soka Tanzania Bara, Yanga na Simba baada ya kufungwa kwa dirisha hilo la usajili h… Read More
  • Rasmi: Torino Yamnasa Joe Hart Mlinda Mlango namba moja wa Uingereza Joe Hart amekamilisha uhamisho wa kujiunga na Klabu ya Torino inayoshiriki ligi kuu nchini Italia kwa mkopo akitokea Manchester City. Hart alijikuta akiwa chaguo la pili la kocha Pep … Read More
  • Arsenal Yakamilisha Usajili Wa Shkodran Mustafi Klabu ya Arsenal imetangaza rasmi kumsajili beki wa kati wa Valencia Shkodran Mustafi kwa ada ya uhamisho ambayo haijawekwa wazi. Licha ya thamani ya uhamisho wa mchezaji huyo kutowekwa wazi lakini habari za chini chini z… Read More
  • Rasmi:Samir Nasri Atua Sevilla Manchester City imetangaza kuwa Samir Nasri amejiunga na klabu ya Sevilla kwa Mkopo. Endelea Kuungana Na Soka24 kwa habari za papo kwa papo za Soka kote Ulimwenguni............. ================== Stori Kubwa Zinazotikisa… Read More

0 comments:

Post a Comment