Thursday, June 1, 2017

Man City Yaweka Rekodi Ya Dunia Kwa Usajili Huu

Klabu ya Manchester City imefikia makubaliano ya kumsajili mlinda mlango Ederson Moraes kutoka katika klabu ya Benfica ya nchini Ureno kwa kitita cha paundi milioni 35. 


Uhamisho wa kipa huyo mwenye umri wa miaka 23 wa thamani hiyo ya fedha unamfanya Ederson kuwa kipa ghali zaidi kuwahi kusajiliwa kwa thamani hiyo ya pesa katika historia ya mpira wa miguu baada ya Gianliugi Buffon aliposajiliwa na Juventus akitokea Parma mnamo mwaka 2001.

Ederson alisafiri kwenda Manchester Jumatatu na Jumanne alitua katika uwanja wa mazoezi wa City kukamilisha vipimo vya afya na kufanya mahojiano na vyombo vya habari vya klabu.
City sasa wanakuwa wameshatumia kitita cha paundi milioni 78, baada ya klabu hiyo kumsajili kumnasa kiungo Bernardo Silva kwa kitita cha paundi milioni 43 kutoka Monaco.

Historia yake kwa ufupi;

Related Posts:

  • SHIZA KICHUYA ATUA MSIMBAZI Klabu ya Mtibwa Sugar imethibitisha kukamilisha uhamisho wa mchezaji wao Shiza Kichuya kujiunga na klabu ya Simba. Kwa muda mrefu kichuya alikuwa akihusishwa na kujiunga na wekundu hao wa Msimbazi lakini taarifa za hivi p… Read More
  • WACHEZAJI 10 MBADALA WA PAUL POGBA MAN U Klabu ya Manchester United ipo katika harakati za kuhakikisha wanainasa saini ya Kiungo wa Juventus Paul Pogba, lakini mbio hizo zinaweza kukumbwa na changamoto na hatimaye Man U kujikuta wakishindwa kupata huduma ya nyota h… Read More
  • JAMES RODRIGUEZ AITAJA KLABU ANAYOTAKA KUHAMIA James Rodriguez amesema anataka kujiunga na wababe wa soka la Ufaransa klabu ya Paris Saint-Germain msimu ujao. Rodriguez alikuwa akihusishwa sana kutimkia ligi kuu ya Uingereza lakini amesema anatamani kujiunga na PSG. … Read More
  • MNIGERIA AHMED MUSA ATUA LEICESTER CITY Klabu ya Leicester City imemsajili mshambuliaji wa Nigeria Ahmed Musa kutoka CSKA Moscow kwa mkataba wa miaka 4 utakaogharimu pauni milioni 16. Southampton,Everton na West Ham walikuwa wakitafuta saini ya mchezaji huyo. M… Read More
  • TISA WAONGEZEWA MKATABA NDANDA FC Timu ya Ndanda Fc imewaongezea mkataba wa mwaka mmoja wachezaji tisa kwa ajili ya kuendelea kukitumikia kikosi hicho msimu ujao wa Ligi Kuu Vodacom 2016/17. Msemaji wa Ndanda Fc, Idrisa Bandali aliwataja wachezaji walioon… Read More

0 comments:

Post a Comment