Saturday, February 11, 2017

Samatta atupia bonge la goli Pro League, avunja rekodi ya Kevin De Bruyne



Timu ya Genk jana imeilaza timu inayoshika nafasi ya 11 ya Msimamo wa ligi kuu nchini ubeligiji maarufu kama Belgium Pro League ya St.Truiden kwa jumla ya goli 3 – 0 katika dimba la Staaien.

Dakika ya 37 milango ya magoli ilianza kufunguliwa pale Alejandro Pozuelo alipomalizia kazi nzuri kutoka kwa Siebe Schrijvers.

Dakika 2 (37’) badae mtanzania Mbwana Ali Samatta aliiandikia timu yake goli la pili  na goli lake 18 ndani ya kilabu hiyo na hivyo kuvunja kabisa rekodi ya mchezaji wa Manchester City ya nchini England Kevin De Bruyne ya kuwa na goli 17 katika misimu yake alipokuwa anaitumikia timu ya Genk.

Sasa Samatta ankuwa ni mchezaji wa 14 wa miaka yote mwenye goli nyingi katika historia ya kilabu ya Genk.


Dakika 45 Ruslan Malinovsky alihitimisha karamu hiyo ya magoli pale alimalizia kazi ya Leandro Trossard.


Mpaka mwisho wa mchezo wenyeji St.Truiden 0 – 3 Genk, kwa Matokeo hayo Genk sasa imefikisha pointi 41 baada ya michezo 26 huku kinara wa ligi hiyo akiwa ni Club Brugge yenye pointi 52 baada ya michezo 25.

0 comments:

Post a Comment